MKUU wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania(TCRA)
Kanda ya Ziwa Mhandisi Francis Mihayo ametoa
wasilisho la chaneli za maudhui ya bila kulipia kwa
madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato.
Akizungumza mbele ya madiwani hao leo Mhandisi
Mihayo amewaambia madiwani hao mkakati wa TCRA
ni kuhakikisha wenye visambusi wanafuata leseni zao ili
kutoa fursa kwa Watanzania kupata haki ya kuona
chaneli kama ambavyo leseni zinavyoelekeza.
Hivyo amewataka madiwani hao kuwaeleza wananchi
kuhusu visambusi ambavyo wanatakiwa kununua na ili
kuona chaneli zote muhimu bila kulipia.
"Madiwani wetu tunawaomba muwaambie
wananchi wanunue visambusi vya TING,
DigTeck,Startimes na Contineto ambavyo ndivyo
vyenye leseni ambazo zinawapa uhalali wa kuonesha
chaneli za nyumbani,"amesema Mhandisi Mihayo.
Amefafanua baada ya kuona kuna wamiliki wa
visambusi wanakiuka taratibu ilifunguliwa kesi
mahakamani na baada ya kushinda wakaona ni vema
watu wakaumia alau kidogo lakini kurudisha utararibu
ambao upo kisheria katika kuonesha chaneli za
nyumbani.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...