Na Emmanuel Massaka, Blogu ya jamii
MBUNGE wa Mkuranga na Naibu Waziri wa mifugo na uvuvi Abdallah Ulega ameendelea na ziara ya kukagua na kuhamasisha miradi ya mandeleo pamoja na kusikiliza kero za wananchi.
Akizungumza na wananchi wa Nganje ulega amesema kuwa maisha ni ya kutegemeana baina ya wavuvi na wakulima hasa katika kujenga uchumi wa nchi.
Aidha amesema kuwa lazima wanakijiji lazima watambulike katika vijiji wanavyoishi na kuishi kama familia na kuheshimu kamati za masuluhisho kwa kuwa hakuna sababu za kuishi kwa kuhitilafiana.
Aidha Ulega amesema kuwa suala la amani na kuishi kwa amani,na ameagiza kata ya Magawa kwa mwezi mmoja kuwatambua wasiotambulika katika vijiji vyao.
Kwa upande wake mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Juma Abeid amesema kuwa halmashauri wametenga kiasi kama cha shilingi milioni 20 kwa ajili ya ujenzi wa zahanati hiyo.
Aidha kuhusu bima ya afya amewashauri wananchi kutumia fursa iliyopo katika kuhakikisha suala la afya linapewa kipaumbele kwa kuwa sasa limerahisishwa kwao.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi (Mb) wa Mkuranga,Abdallah Ulega akimkabidhi Mwenyekiti wa halmashauri na Diwani kata ya Magawa, Juma Abed vitanda viwili vya kujifungulia.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,(Mb)wa Mkuranga,Abdallah Ulega akimkabidhi Mwenyekiti wa halmashaul ya Mkuranga,Juma Abed mabati kwaajili ya ujenzi wa kituo cha afya kata ya Magawa Wilaya Mkuranga mkoa wa Pwani.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi na (Mb) wa Mkuranga, Abdallah Ulega akiwa kwakushiriki na Mwenyekiti Halmashaul wakikabidhi vijana wa kata ya Magawa mipila kumi kwaajili ya mazoezi.
(Picha na Emmanuel Massaka wa Globa ya jamii)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...