WAFANYAKAZI benki ya TIB Corporate leo wamemtembelea mteja wake ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) Waziri Waziri Kindamba.

Wafanyakazi hao wamemtembelea kwajili ya kujitathmini juu ya huduma zao katika wiki ya huduma kwa wateja ambayo hufanyika kila ifikapo Oktoba kila mwaka.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) Waziri Waziri Kindamba akizungumza na MICHUZI BLOG amewashukuru benki ya TIB kwa kufanya kazi kwa ufanisi pamoja na uaminifu.

Pia amewapongeza kwa kufika ofisini kwake na ka kufanya kazi kwa vitendo sio kukaa ofisini na kuwashukuru wateja wake.
Mfanyakazi wa benki ya TIB Corporate, Grace Wilbard akimpa ua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) Waziri Waziri Kindamba wakati alipotembelewa na wafanyakazi wa wa benki ya Tib Corporate jijini Dar es Salaam leo ikiwa ni njia moja wapo ya kusheherekea wiki ya huduma kwa mtaja ambayo hufanyika kila oktoba.
 Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) Waziri Waziri Kindamba akizungumza na wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate jijini Dar es Salaam leo na kuwashukuru kwa kazi wanayoifanya benki hiyo.

Mkurugenzi wa idara ya sheria benki ya TIB Corporate Edward Lyimo  akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) Waziri Waziri Kindamba kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya biashara wa benki ya TIB Corporate Mwallu Mwachin'ga Kushoto ni Mkurugenzi idara ya uendeshaji wa benki ya TIB Corporate.
Wafanyakazi wa benki ya TIB Corporate wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL Corporation) Waziri Waziri Kindamba jijini Dar es Salaam leo walipomtembelea ofisini kwake ikiwa ni kusheherekea wiki ya huduma kwa wateja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...