Na WAMJW-DODOMA

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, imewaasa Watanzania kujijengea tabia ya kupima macho mara kwa mara ili kuweza kuepuka aina mbalimbali za magonjwa ya macho ikiwemo vikope.

Hayo yamesemwa na Kaimu Mganga Mkuu wa Serikali Dkt. Eliud Eliakimu wakati wa kufungua hafla ya kuelekea siku ya Afya ya Macho Duniani ambayo huadhimishwa kila alhamisi ya Pili ya mwezi Octoba.“Asilimia kubwa ya magonjwa ya macho yanatibika ikiwemo upeo mdogo wa macho kuona  ambao yanazuilika kwa miwani  endapo mtu akiwahi katika kituo cha kutolea huduma za Afya na akigundulika ana tatizo la macho basi atapata matibabu mapema”alisema Dkt. Eliakimu.

Aidha, Dkt. Eliakimu alisema kuwa kwa Tanzania watu wasioona kabisa ni asilimia moja sawa na watu laki 5.7 huku watu wenye matatizo mbalimbali ya macho wanakadiriwa kuwa mara tatu ya wasioona kabisa sawasawa na mil.7.Kwa mujibu wa Dkt. Eliudi amesema kuwa takwimu zinaonesha kwamba ugonjwa wa macho umepungua kutoka asilimia 4.6 mwaka 1990 na kufikia asilimia 3.4 mwaka 2015 kutokana na hamasa ya juu ya upimaji toka kwa wananchi.

Kwa upande wake Kaimu Meneja Mpango wa Huduma za Macho Nchini kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Benadertha Chilio amesema kuwa tatizo la macho linaloongoza nchini ni mtoto wa jicho ambapo wagonjwa wanafikia kwa asilimia 50 na wengi wao ni wanawake.
 Kaimu mganga mkuu wa serikali Dkt. Eliud Eliakim (Kushoto) akimkabidhi Kaimu Meneja wa Mpango  wa Taifa wa huduma za macho Dkt. Bernadetha Chilio kitabu cha muongozo wa utoaji huduma za macho katika maadhimisho ya wiki ya afya ya macho yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere jijini Dodoma.
DSC_0615
Washiriki kutoka taasisi mbalimbali za serikali na sekta binafsi wakiwa katika maandamano kuadhimisha wiki ya afya ya macho yaliyofanyika jijini Dodoma mapema leo.
DSC_0719
Kaimu Mganga Mkuu Wa Serikali Dkt. Eliud Eliakim akipata maelezo kutoka Titus Nyange jinsi mashine ya Perkins inavyochapa nukta nundu zinazosomwa na watu wenye ulemavu wa macho wakati wa maadhimisho ya wiki ya afya ya macho duniani yanayofanyika jijini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...