*Ni baada ya Hospitali ya macho ya Dk Agarwal kuamua kufanya uchunguzi bila malipo
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
WATU zaidi ya 300 wamefanyiwa uchunguzi wa macho yao na matatizo mbalimbali yamegunduliwa ambayo husababisha uoni hafifu au upofu huku pia ukitolewa ushauri wa namna ya kutunza macho.

Hivyo kati ya hayo yaliyogundulika, yamejumuisha magonjwa ya mtoto wa jicho, mzio wa macho, matatizo ya kisukari yalioathiri macho, presha ya macho na mengine. Uchunguzi huo umefanywa na Hospitali ya macho ya Dk Agarwal ambayo imeamua kutoa huduma ya upasuaji kwa wagonjwa waliobainika kuwa na matatizo ya macho, hasa kwa wale wagonjwa wenye mtoto wa jicho bila tozo yoyote.
Uamuzi huo ni kama mchango wake katika jamii katika harakati za kupunguza na kuondoa mzigo wa upofu hapa nchini Tanzania na Duniani kwa ujumla. 


Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Daktari Bingwa na Mshauri wa magonjwa ya macho na upasuaji wa Retina katika hospitali hiyo Dk. Emeritus Chibuga. Amefafanua kuwa Hospitali ya macho ya Dakta Agarwal, kama mdau wa kutoa huduma ya macho hapa Tanzania, imetoa huduma za uchunguzi wa macho kwa wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam katika Hospitali ya Mwananyamala

Amesema kuwa mbali ya kutoa huduma za tiba kwa wagonjwa wote wenye mahitaji makubwa na wasio na uwezo pia Hospitali ya Macho ya Dk Agarwal imetoa ushauri unaohusu afya ya macho kwa watu waliojitokeza kupimwa macho yao na kuwafahamisha 
dalili za hatari zinazoweza kuashiria shida za macho.
Kusoma zaidi BOFYA HAPA.
 Dk. Emeritus Chibuga na Dr. Huzeifa kutoka hospital ya macho ya Dkt. Agarwal wakizungumza na mmoja wa watu walioenda kupata huduma ya kupima macho katika hospital ya Mwananyamala jana katika kuadhimisha siku ya macho duniani.
 Daktari mtaalam wa masuala ya macho kutoka hospital ya Dr. Agarwal iliyopo jijini Dar es Salaam akimpatia maelekezo kijana aliyefika kupatiwa huduma ya kupima macho.
Daktari akimpima mmoja wa wagonjwa wa macho aliyefika katika hospital ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam. Hospital ya Dr. Agarwal imetoa huduma ya upimaji na ushauri bure kwa watu mbalimbali wanaosumbuliwa na matatizo ya macho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...