*Atoa miezi miwili Wizara ya Habari ikamilishe mchakato wa vazi la Taifa

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa muda wa miezi miwili na nusu kwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezoiwe imekamilisha mchakato wa Tanzania kuwa na vazi la Taifa.

Amesema Watanzania bado hawajaunganishwa kwa kuwa na vazi la Taifa, ambalo mchakato wake  umeendeshwa kwa miaka mingi na wizara hiyo bila ya kujulikana wamefikia wapi.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumamosi, Oktoba 13, 2018) wakati akifunga tamasha za Urithi Festival, lililofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid Jijini  Arusha.

“Ifikapo Desemba 30,2018 tuwe tumeanza kupata sura ya vazi la Taifa ili wadau walijadili na waamue ni vazi gani la Mtanzania ambalo litawakilisha Taifa kama nchi nyingine walivyomudu kuwa na vazi la Taifa.”

Aliongeza kuwa ili kufikia azma  Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezoiandae tamasha maalumu kwa ajili ya kuonesha aina tofauti za nguo ili kupata vazi la Taifa.

Kadhalika, Waziri Mkuu aliwaagiza waandaaji wa tamasha la Uridhi Festival wahakikishe kuanzia  mwakani kuwe na uratibu wa pamoja baina ya Tanzania Zanzibar na Tanzania Bara ili tamasha lifunguliwe upande mmoja na kufungwa upande mwingine wa Muungano.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akiwahutubia wananchi waliyohudhuria wakati wa kufunga Tamasha la Urithi, lililofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Oktoba 13, 2018.
 Naibu Waziri Maliasili na Utalii Josephat Hasunga, akizungumza na wananchi waliyohudhuria kwenye Tamasha la Urithi, lililofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Oktoba 13, 2018.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipokea maandamano, katika Tamasha la Urithi, lililofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Oktoba 13, 2018.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akitembelea banda la Maliasili na Utalii katika Tamasha la Urithi, lililofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Oktoba 13, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa na mkewe Marry, akiangalia bidhaa ya asili katika banda la wajasiriamali katika Tamasha la Urithi, lililofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Oktoba 13, 2018, kutoka kushoto ni Bibi Eliamulika Ayo, Naibu Waziri Maliasili na Utalii Josephat Hasunga.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, akipokea zawadi ya ngoma na kikombe kutoka kwa Mwenyekiti wa Kikundi cha Wasanii Arusha Fred Thomas, wakati akikagua mabanda kwenye Tamasha la Urithi, lililofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Oktoba 13, 2018.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa na mkewe Marry, wakiangalia bidhaa ya bidhaa iliyobuniwa na mwanadada Glory Silayo (kushoto), katika Tamasha la Urithi, lililofanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha Oktoba 13, 2018.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...