Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

KAMPUNI saba kutoka nchini Uturuki zimekuja nchini Tanzania na kuonesha nia ya kuwekeza katika ujenzi wa maduka makubwa ya nguo, uwekezaji katika sekta ya nishat ya umeme, hoteli zenye hadhi ya nyota tano katika Jiji la Dodoma na uuzaji wa bidhaa.

Ujio wa kampuni hizo ni muendelezo wa jitihada zinazofanywa na Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) kwa kushirikiana na wadau katika kuhakikisha wanaendelea kuhamasisha nchi mbalimbali kuja kuwekeza nchini.

Akizungumzia ujio wa Kampuni hizo kutoka nchini Uturuki,Balozi wa Tanzania nchini Uturuki Elizabert Kiondo amesema nchi yetu kwa sasa ipo kimkakati katika kuelekea uchumi wa viwanda na hivyo ujio wa kampuni hizo ambazo zitawekeza n chini zitasaidia kuongeza juhudi kwa vitendo.

Amesema nchi ya Uturuki inatambua hali tulivu ya n chini Tanzania katika masuala ya uwekezaji na hivyo moja ya jukumu ambalo amelifanya ni kuhamasisha kampuni mbalimbali za nchi hiyo zinakuja kuwekeza kwa maslahi ya Watanzania wote."Nchi yetu ipo kwenye mkakati madhubuti wa kuhakikisha tunaimarisha uchumi wetu kupitia viwanda na uwekezaji.Wenzetu wa Uturuki wameelewa tunakoelekea na hivyo sasa wamekubali kuja nchini kuwekeza.

" Hizi kampuni saba ambazo nimekuja nazo zimeonesha nia ya kuwekeza kwenye maduka makubwa ya nguo, kujenga hoteli zenye hadhi ya nyota tano,kushiriki kwenye sekta ya umeme na kuongeza thamani ya bidhaa zitokanazo na kilimo,"amesema Balozi Kiondo.

Amefafanua kuwa kampuni hizo zimeonesha kuamini Tanzania kuna soko la uhakika na kubwa zaidi baada ya kuanza shughuli zao hakutakuwa na sababu ya msingi kusafiri kwenda katika nchi hiyo kupata bidhaa kwani zitapatikana hapa hapa nchini Tanzania.Kwa upande wake Mkurugenzi wa Uhamasishaji Uwekezaji kutoka Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC)John Mnali amesisitiza kampuni hizo saba kuonesha nia ya kuwekeza nchini katika nyanja mbalimbali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...