Jopo la Madaktari bingwa na wataalamu wa magonjwa ya watoto wamefika katika Hopitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya kuendesha kambi ya matibabu ya hiyari kwa watoto wadogo na wachanga wanaozaliwa katika Wodi ya Watoto ya Hospitali ya Muhimbili.
Kambi hii ya matibabu itadumu kwa muda wa juma moja kuanzia tarehe 5 Novemba. 2018.
Madaktari hawa wamekuja Tanzania kwa mpango wa matibabu ya hiyari unaoratibiwa na Ubalozi wa Tanzania nchini Saudi Arabia, Taasisi ya Misaada ya Kijamii ya PELEKS na Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Kambi tiba kama hii hufanyika mara nne kwa mwaka.
Pamoja na kufanya matibabu ya bure kwa watoto pia madakatari hawa wamekuja na vifaa tiba kadhaa zikiwemo ventilators ambavyo vimetolewa msaada kwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutoka King Faisal Specialist Hospital (KFSH) ya Riyadh.
  Madaktari bingwa kutoka Saudi Arabia wakiwa kazini na madaktari wenyeji katika wodi ya watoto kambi hii ya matibabu itadumu kwa muda wa juma moja kuanzia tarehe 5 Novemba  2018.
 Baadhi ya Madaktari Bingwa kutoka Saudi Arabia wakijadiliana na madaktari wenyeji wa Wodi ya watoto.
 Maelekezo na majadiliano yakiendelea.
 Mmoja wa Wataalamu kuto Saudi Arabia akitoa maelezo mafupi kwa watendaji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kambi hii ya matibabu itadumu kwa muda wa juma moja kuanzia tarehe 5 Novemba. 2018.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...