Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha

Imeelezwa kwamba tabia ya wazazi kutoa ahadi ya zawadi kwa kila wanachofanya watoto wao ni kibaya na kinawajengea mazingira magumu watoto hao baadae hasa pindi hali ya uchumi inapobadilika.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Kitengo cha Dawati la Jinsia na Watoto mkoa wa Arusha Inspekta Happyness Temu wakati alipokuwa anafafanua aina za malezi katika kipindi cha Jambo Tanzania kinachorushwa hewani kila siku Asubuhi katika kituo cha Redio cha Triple “A” kilichopo jijini hapa.

Inspekta Happyness alisema kwamba, baadhi ya wazazi wamekuwa na tabia ya kutoa ahadi ya fedha au vitu kwa watoto wao kwa nia ya kutoa hamasa ili wafanye vizuri aidha katika masomo au shughuli zozote hali ambayo kimalezi si sahihi kwani inaweza kusababisha mtu kuwa tabia tofauti pindi atakapokuwa mkubwa.

“Tabia hii inawafanya watoto wanapokuwa kwenye malezi wawe na matumaini kwamba kila kizuri wanachofanya lazima mwishoni kiendana na zawadi na hivyo mtoto anasababishiwa tamaa, mfano ukimaliza ugali wote nakununulia keki”. Alisema Inspekta Happyness.

Alisema pindi anapokuwa mtu mzima hali hiyo itamuathiri kwa kuwa atakuwa anataka kupewa asante ya kitu au fedha kutoka kwa kila atayemhudumia mara baada ya kumaliza kazi kitu ambacho si sahihi.

Alisema pongezi kwa mtoto sio lazima iendane na kuahidiwa na kupewa kitu au fedha bali inaweza kufanyika kwa njia ya maneno tu na ikamridhisha kwani si kila wakati mzazi unaweza ukawa na uwezo ule ule kiuchumi kuna wakati unashuka au mtoto anakuwa mikononi mwa walezi wengine ambao uwezo wao ni mdogo.
Pichani ni Mkuu wa Kitengo cha dawati la Jinsia na Watoto mkoa wa Arusha,Inspekta Happyness Temu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...