KASKAZINI Mashariki mwa hifadhi ya Mlima Kilimanjaro kuna mti mrefu kuliko yote Afrika. Mti huo wenye kilometa 81.5 unapatikana katika moja ya bonde la mlima huo.

Kulingana na utafiti uliofanywa na mwanazuoni Adreas Hemps toka Chuo kikuu Bayreuth nchini Ujerumani akinukuliwa na jarida la Biodeversity and Conservation ambalo limeeleza kuwa Andreas aligundua mti huo miaka 20 iliyopita katika hifadhi hiyo na baadaye kati ya mwaka 2012 na 2016 alikuja na wataalamu wenzake na kuupima urefu wake ambapo kutokana na vipimo hivyo walikadiria umri wa mti huo ni kuanzia miaka 500 hadi 600.

Mti huo unaojulikana kwa jina la Colossus umevunja rekodi ya dunia kwa urefu wake na uliwahi kufananishwa na mti aina ya Sydney uliopo Limpopo Afrika Kusini ambao ulikufa mwaka 2006.

Pia fahamu kuwa mlima Kilimanjaro ndio mlima mrefu zaidi duniani kwa milima isiyo na safu na una kilele chenye mita 5895 kutoka usawa wa bahari ukiwa na vilele maarufu vya Kibo na Mawenzi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...