Na Ahmed Mahmoud Arusha

Shirika la taifa la Tafa (NHC)Limewataka wale wote walikabidhiwa hati za viwanja walivyopewa katika la eneo la Safari City lililopo kata ya Mateves nje kidogo ya jiji la Arusha kuhakikisha wanaendeleza maeneo yao ili kuhakikisha huduma muhimu za umeme na maji zinasogezwa katika mji huo mpya.

Akizungumza katika hafla ya makabidhiano ya Hati ya umiliki wa eneo na kibali cha ujenzi kwa mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira(AUWSA) iliyofanyika katika kata ya matever jijini hapa Mkurugenzi wa shirika la nyumba la taifa(NHC)Dkt.Maulidi Banyani amesema kuwa shirika hilo katika kuhakikisha linafikia malengo ya kusogeza huduma zake kwa jamii ya watanzania wa vipato vyote na kupunguza gharama za ujenzi kuendana na mazingira.

Ameeleza kuwa limeingia makubaliano na AUWSA na kuwapatia eneo lenye ukubwa wa squaremita elfu 13 kwa ;lengo la ujenzi wa ofisi kuu ya kanda,Karakana,Bohari na Kituo cha Taarifa za mita hatua hiyo itasaidia kupunguza tatizo la maji katika eneo hilo baada ya mamlaka hiyo kuonyesha nia ya kusogeza huduma hiyo kupitia mradi huo.

Kwa upande wake Kaimu mkurugenzi wa AUWSA Mhandisi Humphrey Mwiyombela amelishukuru shirika la nyumba kwa kuwapatia eneo hilo nakuhaidi kujenga jengo lenye ukubwa wa ghorofa sita litakalotumika kama ofisi kuu ya kanda ambalo litafungwa mitambo maalumu ya kupokea taarifa za mbali mbali katika mtandao wao wa huduma za maji.
Mkurugenzi wa shirika la nyumba la taifa Dkt.Maulidi Banyani akiwa na Kaimu mkurugenzi wa Auwsa Mhandisi Humphrey Mwiyombela wakikabidhiana hati ya kiwanja na kibali cha ujenzi wa ofisi za AUWSA kwenye eneo la Safari City nje Kidogo ya jiji la Arusha Picha na mahmoud ahmad wa globu ya jamii Arusha.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...