Katika maeneo mengi ya Tanzania bado kumekuwa na vitendo vya unyanyasaji na ukatili wa kijinsia ambapo wasichana wengi wamekuwa wakiolewa katika umri mdogo, wengine wakibakwa na wengine kupata ujauzito huku wakiwa bado wanafunzi.
Hili ni janga kubwa lakini bado wasanii wengi wamekuwa wakilikaushia, ila kwa ujasiri na kuthubutu, mabinti hawa wameamua KUSEMA na kulizungumzia. Wimbo ambao umezalishwa na Tanzania Bora Initiative na Producer Mocco Genius na video kufanywa na Hascana. Okoa mtoto wa kike, okoa jamii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...