Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza wakati akitangaza uamuzi wa Serikali kununua korosho zote za wakulima msimu huu kwa bei ya shilingi 3,300 kwa kilo baada ya wanunuzi binafsi kushindwa kutimiza maagizo ya Serikali kwa kuanza kununua kwa kusuasua na kwa bei isiyoridhisha.
Uamuzi huo aliutoa wakati akizungumza na viongozi
mbalimbali wa Serikali mara baada ya kuwaapisha Viongozi saba wakiwemo Mawaziri
wawili, Naibu Mawaziri wanne, pamoja na Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha
Sheria, Jumatatu Novemba 12, 2018 Ikulu jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...