Na Ahmed Mahmoud Arusha
Jaji mstaafu wa makahama kuu Aishieli Sumari Ameitaka serikali kuhakikisha kuwa ina weka mazingira mazuri kwa kupata kinga kwa wale wanaosikiliza kesi katika mahakama nchini kwa kuangalia ni namna gani vielelelzo vinavyotunzwa ili mwisho wa siku kinapofunguliwa kisiwadhuru wahusika ndani ya mahakama.

Aidha Amewataka majaji nchini kuhakikisha wanatafsiri  Sheria na kuzitolea adhabu zinazoendana na makosa yatakayoonekana kama Adhabu kwa wahusika badala ya kuziona adhabu kama sehemu ya kuondoka eneo moja kwenda jingine na kujikuta wahusika wakitumia fedha za serikali bure kwenye magereza.

Jaji Sumari ameyasema hayo wakati wa Misa ya Shukran iliyofanyika katika Kanisa la Kilutheri usharika wa Patandi wilayani Arumeru ambapo alitolea mfano wa Adhabu aliyotoa hivi karibuni kabla ya kustaafu ya Usafirishaji wa Madawa ya Kulevya aina ya Mirungi na kumuhukumu mshtakiwa Kifungo cha maisha.

 Amesema kuwa japo alikuwa akitoa adhabu za kifungo cha maisha na kunyonga kwa kesi moja katika maisha yake ya kasi ila sehemu kubwa ya vifungo hivyo vinaipotezea serikali fedha nyingi kwani naamini kuwa kumfunga mtu maisha ni kumuhamisha mtu sehemu moja akizoea anakuwa anakula bure na kuwa huru kwa kuwa anakuwa ameyazoea mazingira hayo.

Akagusia kesi ya kifungo cha maisha yaliyoihukumu kabla ya kustaafu kwa kuzungumzia sheria aliyoshitakiwa nayo inasemaje kwa kuwa sheria hii mpya imembana mwamuzi kwani sheria haina mbadala kwani yeye kama jaji haamini katika kutoa adhabu kubwa ndio kutoa adhabu bali hukumu ndio ionyeshe adhabu iliyotolea.

“Alisema kuwa vielelezo katika kesi za madawa ya kulevya zimekuwa zikichukuwa muda mrefu na kutumia fedha nyingi kwa kuhakiki vielelezo na utunzaji ambapo wakati vielelezo vinapatikana gharama zinakuwa kubwa na kuigharimu serikali”alisema Jaji Sumari.

Akaitaka serikali kuhakikisha kuwa ina weka mazingira mazuri kwa kupata kinga kwa wale wanaosikiliza kesi hizo kwa kuangalia ni namna gani vielelelzo vinavyotunzwa ili mwisho wa siku kinapofunguliwa kisiwadhuri wahusika ndani ya mahakama.

Amewataka Mahakimu na majaji wote kusimamia Haki na wajibu sheria katika siku zote kwa kusimama kwenye viapo vyao kwa kutopemndelea upande wowote kwa kuangalia kuwa kiapo hakiishii kwenye siku ile moja kina upana wake na kusimamia sheria inavyosema kwa kusimamia Haki.

“Sheria na haki zitakaposimamiwa vizuri wananchi wataiona mahakama kama kimbilio lao hivyo nawasihi wenzangu katika kutafisiri sheria waangali viapo vyao kwa kutoa adhabu ambazo wengi wataona adhabu hizo kama kumkomoa mtu bali ni fundisho kwa kuangalia mazingira” alisema Jaji Sumary.
Jaji mstaafu wa mahakama kuu kanda ya Moshi akiongea na wanahabari wakati wa Misa ya Shukran iliyofanyika katika Kanisa la Kilutheri usharika wa Patandi wilayani Arumeru.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...