TAARIFA KUHUSU UTHIBITISHAJI WA NYARAKA

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki inapenda kuukumbusha Umma kwamba wale wote wanaohitaji kupata huduma ya kuthibitisha vyeti na nyaraka mbalimbali wanatakiwa kuzingatia mambo yafuatayo:

(1)  Huduma hizo zinatolewa katika Ofisi za Wizara Mjini DODOMA jengo la LAPF, Barabara ya Makole Ghorofa la 6.

(2) Malipo ya nyaraka zitakazothibitishwa yatalipwa kwa njia ya benki, akaunti namba 0150275408200 Foreign Collection Account, CRDB Bank kwa kiasi cha Shilingi Elfu Kumi na Tano tu kwa kila nyaraka (@TSHS 15,000/=). Hati ya malipo ya benki iwasilishwe Wizarani ili kuthibitisha malipo hayo.

(3) Mteja mwenye nyaraka yeyote inayohusu masuala ya talaka, ndoa, hali ya ndoa, tangazo la kuzaliwa, cheti cha kuzaliwa, Cheti cha Kifo, cheti cha ndoa anatakiwa kuanzia ofisi za Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Registration, Insolvency, Trusteeship Agency- RITA) Dar es Salaam.

(4) Vyeti vyote vinavyoletwa Wizarani kwa ajili ya kuthibitishwa, havina budi kupelekwa kwanza katika Taasisi za Tanzania zilizotoa vyeti/nyaraka hizo ili vihakikiwe na kuthibitishwa. Aidha, kwa vyeti au nyaraka zilizotolewa na mamlaka za nchi za nje zinatakiwa kupelekwa kwenye Balozi wa nchi amabayo vyeti hivyo vilitolewa kwa ajili ya uhakiki.

(5) Mteja anayeleta nyaraka za ajira (Mkataba wa ajira) anatakiwa kuanzia ofisi za Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (Tanzania Employment Services Agency –TAESA)

(6)Mteja anayeleta nyaraka iliyo katika lugha tofauti na kingereza anatakiwa kufanya Tafisri ya nyaraka hiyo na kuiambatisha na nyaraka halisi iliyofanyiwa tafsiri. Aidha, tafsiri ya nyaraka ifanywe na BAKITA, BAKWATA na taasisi zilizosajiliwa na kutambulika na Serikali.

(7) Kwa yeyote mwenye Power of Attorney na Deed Poll ahakikishe imesajiliwa na Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi kabla ya kuiwasilisha Wizarani.

(8)Nakala ya nyaraka yeyote inayotakiwa kufanyiwa uhakiki imbatane na nakala halisi ya nyaraka hiyo.

(9)Mteja anatakiwa kuandika barua kwa Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiomba nyaraka hizo zithibitishwe na kueleza matumizi tarajiwa ya nyaraka hizo nje ya nchi. Aidha, Barua ya Katibu Mkuu iambatishwe na nakala (copies) za nyaraka zilizothibitishwa na taasisi husika ambazo zinahitaji kuthibitishwa na Wizara.


WATEJA WOTE WANAOMBWA KUZINGATIA RAI KWAMBA HUDUMA HIZI ZITAKUWA ZINATOLEWA SIKU YA JUMANNE NA ALHAMISI TU, KUANZIA SAA 3.00 ASUBUHI HADI SAA 6:00 MCHANA.

Imetolewa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...