Tanzania kati ya nchi 10 zinazokua kiuchumi ni ya Tisa na Nchi za Kusini Tanzania ni ya Nne na Afrika Mashariki ni ya kwanza ukuaji huo wa uchumi ni kutokana na ripoti ya Benki ya Dunia.

Akizungumza na waandishi habari wakati akitoa Salaam za Rais Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya habari Marketing Dkt. Hassan Abbas amesema kuwa katika miaka mitatu Tanzania imekuwa ikifanya vizuri.

Amesema kuwa katika ukusanyaji mapato umepanda kutoka sh.bilioni 850 mwaka 2015 hadi kufikia sh.Trioni 1.3.Amesema kuna mashirika yameweza kufanya kazi na katika ukusanyaji wa mapato ikiwemo Dawasa , TPA pamoja shirika la Posta.

Dkt. Abbas amesema zaidi ya viwanda 3000 vimesajiliwa na vingine kufanya kazi.Ajira zaidi ya 26000 zimepatikana kutokana na viwanda na kufanya
Kazi ya mahakama ya mafisadi imeanza na kazi mbalimbali zinafanyika .

Upande wa rushwa Tanzania ya pili kwa Afrika Mashariki ya pili katika mapambano ya rushwa.Tanzania imenunua ndege za saba na Nne tayari na Desemba ndege mbili aina ya air bus.

Dkt. Abbas amesema kuwa kuna ujenzi wa reli ya kisasa na iko katika asilimia 35 pamoja na kujenga barabara ya juu ya Tazara huku zingine zikiendelea.Mardi wa stiglers Gorge kuondoa changamoto ya umeme.Amesema serikali imepeleka maendeleo kwa wananchi na sio kuwekea watu fedha mfukoni.
Msemaji wa Serikali na Mkurugenzi wa Idara ya habari Marketing Dkt. Hassan Abbas alipokuwa akizungumza na Wanahabari leo jijini Dar kuhusu miaka mitatu ya Rais Dkt John Pombe Magufuli tangu aingie madarakani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...