Madaktari bingwa wa masikio, pua na koo pamoja na wataalam wengine wakiwa katika picha ya pamoja na watoto 10 waliopandikizwa vifaa vya kusaidia kusikia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH). Wataalam hao leo wamewaona watoto hao wodini ili kujua maendeleo ya afya zao baada ya kupandikizwa vifaa hivyo. Kutoka kulia ni Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Masikio, Pua na Koo kutoka Misri, Prof. Lobna El Fiky, Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Masikio, Pua na Koo, Dkt. Edwin Liyombo wa Muhimbili (aliyembeba mtoto) Kushoto ni mtaalam wa vifaa vya kusaidia kusikia kutoka Misri, Mohamed El Disouky na mtaalam wa usikivu, Fayaz Jaffer na wengine ni wazazi wa watoto hao. Wazazi wa watoto hao wametoka mikoa mbalimbali nchini ikiwamo Kilimanjaro, Songea na Tanga. Hadi sasa idadi ya watoto waliopandikizwa vifaa hivyo imefikia watoto 21.
Watoto waliopandikizwa vifaa vya kusaidia kusikia wakiwa wodini baada ya kupatiwa huduma hiyo.
Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Masikio, Pua na Koo kutoka Misri, Prof. Lobna El Fiky akifuatilia maendeleo ya mtoto aliyepandikizwa vifaa vya kusaidia kusikia na wataalam wa Muhimbili kwa kushirikiana na wataalam kutoka Misri. Kushoto ni Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Masikio, Pua na Koo, Dkt. Edwin Liyombo wa Muhimbili. Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Lawrence Museru na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji wa Muhimbili, Dkt. Sufiani Baruani. Wengine ni wataalam wa magonjwa ya masikio, pua na koo.
Mmoja wa wazazi wa watoto waliopatiwa huduma hiyo akizungumza na Prof. Lawrence Museru wa Muhimbili kuhusu maendeleo ya afya ya mtoto wake. Kushoto ni Prof. Lobna El Fiky.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...