Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

MWENYEKITI wa Jukwaa la wanawake Wilaya ya Mkuranga Mariam Ulega ameendelea na ziara yake iliyolenga kuhamasisha kuwainua wanawake kiuchumi kupitia jukwaa hilo.

Akizungumza na wanawake akiwa ziarani katika kijiji cha Mwandege bi. Mariamu amesema kuwa lengo la kufanya ziara hiyo kuwafahamisha wanawake kuhusiana majukumu yanayofanywa na jukwaa hilo tangu kuanzishwa kwake.

Amesema kuwa akiwa kama mweyekiti wa Wilaya hiyo atahakikisha fursa za kiuchumi zinawafikia ili waweze kuendeleza shughuli zao za kijasiriamali.Kuhusiana na mikopo kwa wanawake bi. Mariamu amesema kuwa wanachotakiwa kufanya ni kuendeleza miradi yao ili waweze kupata mikopo katika halmashauri zao bila riba.

Kwa upande wake diwani wa kata ya Mwandege Adolf Kowero amesema kuwa amekuwa akifarijika na juhudi za akina mama hao na kuhusu ahadi ya eneo alilohaidi kwa ajili ya biashara lipo tayari na ramani imeandaliwa ambapo soko kubwa litajengwa kwa ajili ya wanawake na vijana.

Mwenyekiti wa jukwaa la wanawake wilaya ya Mkuranga,Mariam Ulega akizungumza na wajasiriamali wa kata ya Mwandege ,ambapo amewaomba kufanya kazi kwa waminifu ili waweze kunufaika na kazi zao na kuongeza pato la Taifa.
Diwani wa kata ya Mwandege wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani,Adolf Kowero akizungumza na wajasiriamali wa kata hiyo.
Mwenyekiti wa jukwaa la wanawake wilaya Mkuranga,Mariam Ulega akiwakabidhi viongozi wa kata ya Mwandege laki nne na doti 20 za kanga kwajili ya mtaji wa vikundi mbalimbali vya kata hiyo.
Mwenyekiti wa jukwaa la wanawake wilaya Mkuranga,Mariam Ulega akiwaunga mkono wajasiriamali wa kata ya Mwandege.(Picha na Emmanuel Massaka MMG)
Sehemu ya wajasiriamali wakiwa katika hafla hiyo iliyofanyika katika kata ya Mwandege wilayani Mkuranga Mkoani wa Pwani.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...