Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
BENKI ya CBA kwa kushirikiana kampuni ya simu ya Vodacom wamekabidhi zawadi kwa washindi wake wa promosheni ya shinda na M- pawa katika tawi la benki ya CBA kijitonyama jijini Dar es salaam, na hiyo ikiwa ni baada ya kudumu kwa promosheni hiyo kwa muda wa wiki 6.

Akizungumza katika makabidhiano hayo mwakilishi wa Mkurugenzi wa benki ya CBA Julius Konyani amesema kuwa  promosheni hiyo ililenga kuwafikia wananchi wasiofikiwa na huduma  za kibenki na kuwawekea mazingira ya kujiwekea akiba huku ikiwapa changamoto ya kurudisha mikopo yao kwa wakati pindi wanapochukua mikopo.

Konyani amesema kuwa; "Mikopo yetu ina riba ndogo sana kwani lengo la  kufanya promesheni hii  hasa ilikua ni kuwawezesha kiuchumi wateja wetu, pia promosheni hii ilikua na lengo la kutoa shukrani na kuwazawadia wateja  wetu katika msimu huu wa sikukuu na tumefurahi washindi wetu wamekuwa ishara ya mafanikio yetu katika lengo hili" Ameeleza Konyani.

Aidha amesema kuwa benki ya CBA kwa kushirikiana na Vodacom wataendelea kutoa na kuboresha huduma ya M-pawa na kuwafikia watanzania wengi zaidi wakiwemo wakulima na wajasiriamali ambao watapewa mikopo midogo hadi ya shilingi laki tano ili kuweza kuwapa nguvu katika shughuli zao za kiuchumi wanazozifanya.
Washindi wa bajaji kupitia promosheni ya shinda na M -pawa wakiwa pamoja na baadhi ya viongozi kutoka benki ya CBA na Kampuni ya simu ya Vodacom.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa benki ya CBA Julius Konyani (kushoto)akimkabidhi kadi ya bajaji bi. Mariam Barawa mmoja kati ya washindi watano waliojishindia bajaji hizo kupitia promosheni ya shinda na M- Pawa,  jijini Dar es salaam. Kulia ni meneja masoko wa huduma za kifedha kutoka kampuni ya Vodacom Noel Mazoya. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...