Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kushoto) akimpongeza Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson alipowasili katika uwanja wa ndege wa Mjini Dodoma akitokea Bujumbura, Burundi katika michezo ya Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, Naibu Spika aliongoza msafara wa timu ya michezo ya Bunge. Kushoto ni katibu wa Bunge, Mhe. Stephen kagaigai
Wanamichezo wa timu ya michezo ya Bunge wakipokelewa na uongozi wa Bunge, watumishi wa Bunge wakiongozwa na Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai walipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma wakitokea katika michezo ya Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyofanyika Bujumbura, Burundi
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akipokea cheti cha ushiriki wa michezo ya Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kutoka kwa Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson ambae ni kiongozi wa msafara wa wanamichezo wa timu ya michezo ya Bunge katika michezo ya Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki yaliyofanyika Bujumbura, Burundi katika tukio lililofanyika leo tarehe 10 Desemba, 2018 katika uwanja wa ndege Mjini Dodoma.
Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (mwenye koti nyeusi) akiwa katika picha ya pamoja na wanamichezo wa timu ya michezo ya Bunge walioongozwa na Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson (mwenye tisheti nyeusi) baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Mjini Dodoma wakitokea Bujumbura, Burundi katika michezo ya Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson (katikati) akizungumza na wanamichezo wa timu ya michezo ya Bunge na watumishi wa Ofisi ya Bunge leo tarehe 10 Desemba, 2018 katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma, wakati timu hiyo ilipowasili kutoka Bujumbura, Burundi katika michezo ya Mabunge ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. Ikiwa ni kuwaeleza kwa ufupi mafanikio waliyoyapata katika mashindano hayo na ushirikiano ulioonyeshwa na watumishi wa ofisi ya Bunge kabla na baada ya mashindano

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...