Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
SERIKALI imeagiza amezitaka taasisi zote za na binafsi kuhakikisha wanajisajili kupitia Wakala Afya, Usalama Mahala Pa Kazi (OSHA) ili kutekeleza matakwa ya sheria. Hayo ameyasema Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Kazi Vijana na Ajira Jenista Mhagama alipowatembelea na kuzungumza na wafanyakazi wa OSHA na kuangalia utendaji wao wa kazi katika kusimamia masuala aya usalama mahala pa kazi
Amesema uwepo wa taasisi ya OSHA ni muhimu kwa kuwa inalenga kuondoa dosari za aina mbalimbali hususani madhara katika maeneo ya kazi ambapo bila kufanya hivyo wafanyakazi wangekuwa waadhirika wakubwa katika sehemu za kazi zao.
“Taasisi zote na kampuni kujisajili na OSHA ili ziweze kufanya kazi kwa utaratibu wa kisheria, hii aina maana ina faida kwa Serikali, bali ni faida kwa taasisi , wafanyakazi wote kwa kuwa zaidi imelenga kuhakikisha inaondoa mazingira yote hatarishi ambayo pengine yangeweza kuleta madhara mahala Pa kazi ” amesema Mhagama.
Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Kazi Vijana na Ajira Jenista Mhagama akizungumza na wafanyakazi wa Dawasa walioko katika mafunzo ya Ukimwi yanayoendeshwa na Wakala Afya, Usalama Mahala Pa Kazi (OSHA) wakati alipotembela ofisi za OSHA jijini Dar es Salaam.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa OSHA Hajida Mwenda akizungumza na waandishi habari kuhusiana na usimamizi wafanyakazi mahala pa kazi katika utoaji wa elimu wakati Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Kazi Vijana na Ajira Jenista Mhagama alipotembelea ofisi za OSHA jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wafanyakazi wa Dawasa wakiwa katika mafunzo ya UKIMWI yanayoendeshwa na OSHA jijini Dar es Salaam.
afanyakazi wakiwa katika mkutano na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Kazi Vijana na Ajira Jenista Mhagama alipotembelea ofisi za OSHA jijini Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...