Baada ya Mahakama Kuu kumrejesha kwenye nafasi yake ya Makamu wa Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF) Michael Wambura Novemba 30, leo amewasili ofisini hapo kuripoti kwa mujibu wa Mahakama Kuu.

Wambura amesema kuwa majukumu yake aliyopewa na Mahakama Kuu ameyatekeleza hivyo kwa sasa yeye ni Makamu wa Rais wa TFF kwa kuwa hakufutwa cheo chake bali alifungiwa kutojihusisha na masuala ya soka. 

"Ofisini wengi nimekuta hawapo zaidi ya mkurugeni wa fedha, na wahudumu wengine wa chini, ila kikubwa nimeweza kutimiza masharti ya Mahakama ambayo kwanza ni kuripoti ofisini, pili naleta taarifa ya mahakama ambayo imepokelewa na nimeweza kufika, kama utekelezaji hautafanyika basi nitarejea mahakamani. 

"30 Novemba nilianza kazi baada ya mahakama kuu ilipotoa maagizo, cha msingi ni kwamba nilikuja kutoa taarifa kwamba mimi nipo, walinisimamisha kujihusisha na soka ila hawakufuta cheo changu cha umakamu wa rais," alisema. 

Machi mwaka huu Kamati ya Maadili ya TFF chini ya mwenyekiti wake, Hamidu Mbwezeleni ilimfungia maisha Wambura kutojihusisha na masuala ya soka kwa kumtuhumu kwa makosa matatu. Katika taarifa yake, TFF ilisema kwamba ilichukuwa hatua hiyo kwa mujibu wa kifungu cha 73(1) (c) cha Kanuni za Maadili ya TFF Toleo la 2013. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...