NA MWAMVUA MWINYI, RUFIJI .

NAIBU Waziri wa Ujenzi ,Elias Kuandikwa amemuagiza mtendaji mkuu wa Wakala wa Majengo Nchini (TBA) awasiliane na wizara ya nishati ,kuharakisha upatikanaji wa sh.milioni 800 ili kumalizia ukarabati wa nyumba za makazi 34 zinazojengwa katika ujenzi wa mradi wa uzalishaji umeme wa stiglers gorge Rufiji mkoani Pwani. 

Aidha amemtaka msimamizi wa ujenzi wa nyumba hizo kuhakikisha wanamaliza ujenzi huo wiki nne zijazo. Kuandikwa alielekeza hayo, wakati alipotembelea ujenzi wa barabara kutoka Kibiti -Mkongo na upande wa Mkoa wa Morogoro kupitia Ngerengere hadi Ubena-zote kuelekea kwenye mradi wa stiglers gorge. 

Alisema,wizara kupitia TBA ilikuwa na jukumu la kukarabati maeneo ya makazi na kutakiwa kumaliza mwezi Novemba mwaka huu lakini kutokana na changamoto ya kifedha ujenzi upo hatua ya umaliziaji. ” Nyumba hizi ni muhimu na kuna haja ya kuzikamilisha mapema ili mkandarasi akifika kuanza kazi akute mazingira ya makazi yako vizuri.” 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...