Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
BENKI
ya Commercial Bank of Africa (CBA) kwa kushirikiana na kampuni ya simu
ya Vodacom wamekamilisha rasmi leo kampeni yao "Shinda na M pawa" kwa
kutangaza washindi watano waliojishindia bajaji na mshindi mkuu wa droo
hiyo akijishindia pesa taslimu kiasi cha shilingi milioni 10.
Akimwakilisha
Mkurugenzi mtendaji wa benki ya CBA Hakim Sheikh amesema kuwa benki
hiyo inaendelea kutimiza ahadi kwa wateja wake kwa kuwazadia washiriki
wote walioshiriki katika droo zote zilizofanyika.
Hakim
amesema kuwa, "Kampeni hii imetupa fursa kubwa ya kuwahamasisha wateja
wetu hasa kwa kujiwekea utamaduni wa kujiwekea akiba na tunawahimiza
watanzania ambao bado hawajajiunga na benki ya CBA kujiunga na benki
yetu ili waweze kufaidika na fursa mbalimbali zinazotolewa na benki ya
CBA" ameeleza Hakim.
Hakim
amesema kuwa benki yao itaendelea kutumia teknolojia katika katika
kuhakikisha wanawafikia watanzania zaidi na kuongeza idadi ya wateja
zaidi ya milioni 7 waliopo sasa.
Aidha
amewapongeza washindi 1296 waliopatikana kwenye droo hiyo ya mwisho na
kuahidi kudumisha na kuboresha huduma yao na amewaomba watanzania
waendelee kutumia huduma kutoka benki ya CBA.
Mwakilishi wa Mkurugenzi wa benki ya CBA Hakim Sheikh akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kuchezesha droo ya mwisho ambapo tangu kuanza kwa kuchezeshwa kwa droo hiyo jumla ya washindi 200 kwa kila droo wamepatikana.
Meneja masoko wa Kampuni ya simu ya Vodacom, Noel Mazoya akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuchezeshwa kwa droo hiyo ambapo ameipongeza benki ya CBA kwa kuendesha shindano hilo kwa uadilifu.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...