Na Dixon Busagaga,Morogoro.

WANARIADHA Marko Joseph wa Singida na Amina Mohamed wa JKT –Arusha jana wamewek rekodi mpya baada ya kufanikiwa kushika nafasi ya kwanza kwa mbio za kilometa 21 kwa wananume na wanawake katika mashindano ya Mbio mpya za Morogoro Marathon 2018.

Joseph alifanikiwa kushika nafasi hiyo baada ya kutumia saa 1:05:50 akifuatiwa na mwanariadha Faraja Lazaro w JKT –A rusha aliyemaliza mbio hizo zilizoanzia na kumalizikia katika uwanja wa Jamhuri akituia saa 1:0:04.

Nafasi ya tatu imechukuliwa na mwanariadha mkongwe Dickson Marwa aliyemaliza mbio hizo kwa kutumia saa 1:07:42 huku nafasi ya nne ikichukuliwa na mwanariadha Anthony Moya aliyemaliza mbio kwa kutumia saa 1:07:42.

Kwa upande wa wanawake Amina Mohamed amefanikiwa kushika nafasi ya kwanza baada ya kutumia saa 1:21:47 akifuatiwa n Rozalia Fabiani liyemaliza mbio kwa kutumia saa 1:23:59 huku Monica Nicolaus akishika nafasi ya tatu kwa kutumia saa 2:00:08.

Washindi wa Mbio za Kilometa tano wametangazwa Hashim Athuman (18:50:07) kwa upande wa wanaume huku kwa wanawake akishika nafasi ya kwanza Rosemary Mustapha kutoka mjini Magharibi Zanzibar (23:41:66).
Mgeni rasmi katika Mashindano hayo,Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ,Kebwe Stephen Kebwe akizungumza kabla ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa Mbio za Morogoro Marathoni.
Baadhi ya Washiriki wa Mbio hizo wakimsikiliza Mgeni Rasmi katika Mashindano ya Mbio za Morogoro Marathoni .
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro Kihanga akizungumza katika Mashindano hayo.
Mgeni rasmi katika Mashindano ya mchezo wa Riadha ya Morogoro Marathon ,Mkuu wa mkoa wa Morogoro ,Kebwe Stephen Kebwe akimkabidhi mshindi wa kwanza wa mbio za km 21 kwa wanawake Amina Mohamed zawadi ya king'amuzi cha DSTV.
Mgeni rasmi katika Mashindano ya mchezo wa Riadha ya Morogoro Marathon ,Mkuu wa mkoa wa Morogoro ,Kebwe Stephen Kebwe akimkabidhi mshindi wa tatu wa mbio za km 21 kwa wanawake Monica Nicolaus zawadi ya king'amuzi cha DSTV.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...