NA FREDY MGUNDA,IRINGA.
Migogoro
ya ardhi katika kijiji cha magubike kata ya nzii wilaya ya iringa
imebakia kkama historia baada ya mradi wa feed the future (LTA)
kufanikiwa kupima ardhi na kuwakabidhi hatimiliki ya kimila kwa wananchi
wa kijiji hicho.
Akizungumza
wakatika wa kukabidhi hati hizo za kimila mwenyekiti wa halmashauri ya
iringa Stephen Mhapa alisema kuwa kutolewa kwa hatimikili za kimila
kunamaliza migogoro ya ardhi kwa wananchi wote waliopata hati hizo.
“Sasa
tunaelekea kipindi cha kilimo ambapo ndio kuna kesi nyingi za mipaka ya
ardhi, hivyo uwepo wa mradi huu wa LTA umetusaidia kumaliza kabisa
migogoro ya ardhi naomba kuchukua nafasi hii kwa niaba ya serikali
kuwashukuru kwa kazi mliyoifanya” alisema Mhapa
Mhapa
aliwaomba viongozi wa mradi wa LTA kuhakikisha wanapima vijiji vyote
vya halmashauri ya wilaya ya Iringa ili kuondoa migogoro yote ambayo
imekuwa ikirudisha nyuma maendeleo ya wananchi.
“Kama
serikali ikisema ipime ardhi yote ni kazi nzito,kazi hii ilitakiwa
kufanywa na serkali kutokana na ukosefu wa rasilimali fedha na
rasilimali watu imekuwa tatizo kubwa kwa serikali hivyo lazima mpongezwe
kwa kazi yenu mnayoifanya” alisema Mhapa
Mwenyekiti wa halmashauri ya iringa Stephen Mhapa akiwa na mkurugenzi wa mradi wa feed the future Malaki Msingwa wakati wa kukabidhi hati miliki za kimila kwa wananchi wa kijiji cha Magubike kilichopo kata ya Nzii mkoani Iringa
Mwenyekiti wa halmashauri ya iringa Stephen Mhapa akiwa na mkurugenzi wa mradi wa feed the future Malaki Msingwa wakimkabidhi hati mmoja wa wananchi wa kijiji cha Magubike
Mwenyekiti wa halmashauri ya iringa Stephen Mhapa akiwa na mkurugenzi wa mradi wa feed the future Malaki Msingwa wakicheza nyimbo za asili pamoja na wananchi wa kijiji cha Magubike wakati wa ugawaji wa hati za kimila.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...