Wauguzi nchini wametakiwa kutimiza wajibu wao ili kuhakikisha wanatoa huduma bora kwa wananchi kwa kufuata miongozo iliyopo ikiwamo taratibu, kanuni na sheria.

Hayo yamesemwa na Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania, Bi. Agnes Mtawa katika mkutano wa kikao kazi uliowashirikisha wauguzi wakuu wa mikoa ya Tanzania, wauguzi wakuu wa hospitali za rufaa za kitaifa na hospitali maalum, baadhi ya wakuu wa vyuo vinavyotoa mafunzo ya uuguzi na ukunga pamoja na baadhi ya wauguzi wakuu wa wilaya nchini.

Bi. Mtawa amesema kwamba taaluma ya uuguzi inaongozwa na sheria na kanuni ambazo zimeainisha miongozo jinsi ya kumuwajibisha muuguzi anayekwenda kinyume na taratibu na maadili.“Kutokana na muongozo huu, viongozi wa baraza ngazi ya mikoa, wilaya na vyuo wanapaswa kutimiza wajibu wao katika kusimamia miongozo,” amesisitiza Bi. Mtawa.

Mkurugenzi huyo amewataka wauguzi kuzingatia pia matumizi ya miongozo mipya kama muongozo wa kusimamia utoaji wa huduma ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) uliyoboreshwa yaani NIMART, muongozo wa mafunzo ya kujiendeleza yaani CPD, muongozo wa ufuatiliaji wa huduma za uuguzi na ukunga pamoja na mfumo mpya wa TEHAMA ambao utasaidia kuweka kumbukumbu za huduma zinazotolewa na wauguzi na wakunga kwa kielectroniki.
Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania, Bi. Agnes Mtawa akiwaonyesha washiriki sheria na kanuni inayosimamia taaluma ya uuguzi na ukunga nchini.
Baadhi ya washiriki wakifuatilia kikao hicho ambacho kimefanyika kwenye ukumbi wa ofisi za baraza hilo, Wilaya ya Kibaha, mkoani Pwani.
Msajili wa Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania, Bi. Agnes Mtawa akiwa katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali wa baraza hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...