Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako ameahidi kushughulikia changamoto ya uchakavu wa miundombinu katika vyuo vya ufundi stadi vinavyomilikiwa na VETA ili kuwezesha utoaji wa mafunzo bora sambamba na mabadiliko mbalimbali ya teknolojia viwandani na kukidhi viwango vya mahitaji ya waajiri.

Prof.  Ndalichako alitoa ahadi hiyo kufuatia ombi la Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Dkt. Pancras Bujulu wakati akitoa maelezo mafupi kabla ya kumkaribisha kutoa hotuba kwenye sherehe za mahafali ya 33 ya Chuo cha VETA Moshi yaliyofanyika chuoni hapo Jumatano, 12 Desemba 2018.

Katika maelezo yake, Dkt. Bujulu alisema kuwa baadhi ya vyuo vya VETA ni vikongwe mno na miundombinu yake imechakaa sana, hivyo ukarabati wake kwa kutumia fedha ambazo VETA imekuwa ikipatiwa na serikali umekuwa ni mgumu. Alisema pamoja na uchakavu wa miunndombinu kwa ujumla vifaa na mashine zinazotumika kwenye karakana kwa ajili ya kufundishia pia zimechakaa na zingine  zimepitwa na wakati kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia hivyo hazifai kutumika kufundishia ili kutoa mafundi wanaokidhi mahitaji ya wakati huu.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akitoa hotuba kwenye mahafali ya 33 ya Chuo cha VETA Moshi yaliyofanyika chuoni hapo Jumatano, tarehe 12 Desemba 2018.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Dkt. Pacras Bujulu akitoa Maelezo kuhusu mipango na mikakati ya VETA katika kutoa na kusimamia mafunzo ya ufundi stadi.
 Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akitazama nyaraka za kampuni ya LES Inspection iliyoanzishwa na wahitimu wa VETA ambao wamefuzu na kupata leseni za kutoa ithibati ya kazi za uungaji vyuma kwa kiwango cha kimataifa wakati akitembelea maonesho ya wahitimu kwenye mahafali ya 33 ya Chuo cha VETA Moshi, Jumatano, tarehe 12 Desemba 2018. Kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dkt. Pancras Bujulu na anayefuatia ni Mwenyekiti wa Chemba ya Madini na Nishati, Balozi Ami Mpumbwe.
  Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako akisikiliza maelezo kutoka kwa mhitimu wa fani ya Ufundi wa Kaanga Mvuke (Boiler Mechanics) juu ya mfumo wa kaanga mvuke (Boiler) unavyofanya kazi kwenye mahafali ya 33 ya Chuo cha VETA Moshi, Jumatano, tarehe 12 Desemba 2018. Kulia kwa Waziri ni Mkurugenzi Mkuu wa VETA, Dkt. Pancras Bujulu.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...