RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akinesha Kitabu cha Mtunzi Shafi Adam Shafi cha Mtoto wa Mama, baada ya kukizinduwa leo wakati wa hafla ya Kongamalo la Pili la Kimataifa la Kiswahili lililoandaliwa na Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil ,kulia Waziri wa Vijana Utamaduni Sanaa na Michezo Zanzibar Mhe. Balozi Ali Karume, Katibu Mtendaji wa BAKIZA Bi. Mwanahija Juma na kushoto Mtunzi wa Kitabu hicho cha Mtoto wa Mama Mzee Shafi Adam Shafi akipiga makofi baada ya uzinduzi huo, uliofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akikabidhiwa Vitabu mbalimbali vya Kiu na Nyota ya Rehema na mtunzi wa Vitabu hivyo Ndg. Mohammed Suleiman, wakati wa hafla ya Uzinduzi wa Kongamano la Pili la Kimataifa la Kiswahili Zanzibar, lililofanyika katika ukumbi wa Sheikh Idirissa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimkabidhi Cheti Mtunzi wa Vitabu vya Kuli, Vuta N’kuvute, Haini, Mbali na Nyumbani , Kasiri ya Mwinyi Fuad na Mtoto wa Mama kilichozinduliwa leo.Ndg. Shafi Adam Shafi na kulia Waziri wa Vijana Utamaduni,Sanaa na Michezo Zanzibar Mhe. Balozui Ali Karume, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Mwenyekiti wa Baraza la Kiswahili Zanzibar (BAKIZA) Dkt. Mohammed Seif Khatib, (katikati) wakati akitembelea maonesho ya Vitambu mbalimbali katika viwanja vya Ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil , akiwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, wakiangalia vitabu hivyo.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.Alim Mohamed Shein, akiangalia Vitambu mbalimbali vya Wachapishaji wa Vitabu kutoka Tanzani na Kenya wakati wa maonesho hayo yaliokwenda sambamba na Ufunguzi wa Kongamano la Pili la Kimataifa la Kiswahili LILILOFANYIKA Zanzibar katika ukumbi wa Sheikh Idrissa Abdulwakil Kikwajuni Zanzibar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...