RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akihutubia na kutowa nasaha zake kwa Uongozi wa ZSTC na wananchi waliohudhuria hafla ya kuadhimisha Miaka 50 ya Shirika hilo zilizofanyika jana usiku katika viwanja vya hoteli ya Verde Mtoni Zanzibar.2-12-2018.(Picha na Ikulu).

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akimsikiliza Afisa Masoko wa Shirika la Biashara la Taifa (ZSTC) Nassor Salum Nassor, wakati akitembelea maonesho ya Bidhaa za ZSTC wakati wa maadhimisho ya 50 zilizofanyika katika viwanja vya Hotel Verde Mtoni Zanzibar,kushoto Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein,Mke waMakamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman, Makamu Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif na Waziri wa Biashara na Viwanda Zanzibar Mhe. Balozi Amina Salumu Ali, hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya hotel Verde jana usiku.

MKE wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein, akisalimiana na Mama Fatma Karume, wakati akiwasili katika ukumbi wa hafla ya sherehe za kuadhimisha Miaka 50 ya ZSTC zilizofanyika katika viwanja vya Hoteli Verde Mtoni Zanzibar, jana usiku.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, akiwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar,Balozi Seif Ali Iddi na Mama Mwanamwema Shein, na Viongozi wengi wakiwa wamesimama wakati ukiimbwa wimbo wa Taifa na Kikundi cha Taifa cha Taraab Zanzibar, jana usiku katika hoteli ya Verde Mtoni
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Ali Mohamed Shein, kushoto Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi, Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Unguji Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud na kulia Waziri wa BiashaRA NA Viwanda Zanzibar,Mhe Balozi Amina Salum Ali na Mke wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mama Asha Suleiman, wakifuatilia onesho la “ Documentary “ ya Miaka 50 ya ZSTC,hafla hiyo imefanyika katika viwanja vya hotel Verde Mtoni Zanzibar, jana usiku.
WADAU wa ZSTC wakifuatilia hafla hiyo ya Maadhimisho ya sherehe za Miaka 50 ya Shirika hilo tangu kuazishwa kwake Zanzibar 1968, zilizoadhimishwa katika viwanja vya Hoteli Verde Mtoni Zanzibar, wakimsikiliza Rais wa Zanzibar Mhe. Dk. Shein, akihutubia hafla hiyo, jana usiku. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...