Rais wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhokya amekiri shirikisho hilo kuwa na majadiliano mbalimbali katika ngazi ya Utatu na Upili yaani Serikali, Wafanyakazi na Waajiri kuhusu hoja ya kuunganishwa kwa mifuko ya hifadhi za jamii nchini. 

Akizungumza na waandishi wa Habari mjini Morogoro leo sanjari na vikao vyao vya kikatiba takribani kwa siku mbili, Nyamhokya amesema wajumbe wamekuwa na fursa ya kujadili mambo mbalimbali yanayohusu Ustawi wa Wafanyakazi nchini pamoja na kutoa tamko baada ya kuhudhuria kikao hicho rasmi cha utendaji wa maswala yanayotakiwa kufanyiwa utekelezaji.

Moja ya agenda zilizojadiliwa kwa undani ni swala la uunganiswaji wa wa mifuko ya hifadhi ya jamii na mkanganyiko uliojitokeza baada ya serikali kutangaza kuanza kutumika kwa vikokotoo vya mafao ya pensheni kwa wastaafu wa mifuko ya PSSSF na NSSF kuanzia Agosti 8 2018.
Rais wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Tumaini Nyamhokya akizungumza na wanahabari mjini Morogoro leo, wakati wa kutoa tamko la Kamati ya TUCTA Taifa kuhusu mkanganyiko wa kikotoo cha mafao ya pensheni yatolewayo na mifuko ya Hifadhi ya Jamii Tannzania. Kushoto ni Makamu Rais wa TUCTA, Qambos Sulle, Katibu Mkuu wa Shirikisho hilo, Dk Yahya Msigwa (wa pili kulia) na Naibu Katibu Mkuu Jones Majura. 
Sehemu ya wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), wakimsikiliza Rais wa shirikisho hilo, Tumaini Nyamhokya alipozungumza na wanahabari mjini Morogoro leo, wakati wa kutoa tamko la Kamati ya TUCTA Taifa kuhusu mkanganyiko wa kikotoo cha mafao ya pensheni yatolewayo na mifuko ya Hifadhi ya Jamii Tanzania. 
Sehemu ya wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), wakiimba wimbo wa 'Solidarity Forever' wakati wa mkutano huo. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...