Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Bwana Bernard Konga katika mkutano wa hadhara Halmashauri ya Wilaya ya Nanyamba Mkoani Mtwara wakati wa uhamasishaji wa wananchi kujiunga na NHIF, kupitia Mpango wa Ushirika Afya.

Na Grace Michael

Wananchi Mkoani Mtwara wametakiwa kufanya uwekezaji kwenye afya zao kupitia Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili wawe na uhakika wa kupata huduma za matibabu wakati wowote. Rai hiyo imetolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akizungumza na wananchi katika Halmashauri ya Mji wa Nanyamba mkoani Mtwara.

Amesema kuwa ili kila mwananchi aweze kuwa na uhakika wa kufanya shughuli zingine za maendeleo na uwekezaji mwingine lazima awe na uhakika na afya yake kwa kuwa na uhakika wa kupata matibabu.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akikagua Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mtwara. 

“Nawaomba sana wananchi wa Mtwara wekezeni kwenye eneo la afya zenu na uwekezaji mzuri ni kuwa na Bima ya Afya kupitia NHIF ili iwawezeshe kupata huduma zote za matibabu kwa ngazi mbalimbali za vituo vya kutolea huduma kuanzia ngazi ya Zahanati hadi Hospitali ya Taifa,” alisema Mhe. Ummy.

Alisema kuwa Serikali imeweka utaratibu mzuri wenye gharama nafuu wa kupata huduma za matibabu kupitia NHIF, utaratibu ambao unamtaka mwananchi kujiunga kabla ya kuugua ili aweze kunufaika na huduma za matibabu wakati wowote anapopatwa na maradhi.

“Wengi wetu hapa mmeuza mazao yenu na mnalipwa fedha nyingi, kati ya fedha mnazopata hakikisheni mnatenga shilingi 76,800 tu kwa ajili ya kukata kadi ya bima ya afya ambayo itakusaidia kupata huduma mahali popote ndani ya nchi kwenye zaidi ya vituo 7000 vilivyosajiliwa na NHIF,” alisema Mhe. Ummy wakati akizungumza na wananchi wa Nanyamba Mkoani Mtwara.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu akimhamasisha mmoja wa akina mama kumwandikisha mtoto wake na mpango wa Toto Afya Kadi ili awe na uhakika wa kupata matibabu. 

Aliwahakikishia wananchi upatikanaji wa huduma za matibabu katika hospitali zote nchini kutokana na maboresho makubwa yaliyofanyika chini ya Serikali ya Awamu ya Tano ambayo imeongeza kwa kiasi kikubwa bajeti ya afya hususan bajeti ya dawa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...