*Asema pamoja na ubishi wake lakini amethibitisha Rais Magufuli anastahili sifa,heshima
Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
ASKOFU
Zacharia Kakobe amesema Rais Dk.John Magufuli anafanya mambo makubwa
kiasi cha kwamba amemkosha na kwamba pamoja na ubishi wake kwa sasa
anakubali kazi ambayo inafanywa na Rais.
Amesema
hayo leo wakati amepata nafasi ya kuomba dua ambapo kabla ya kuomba
alianza kwa kuzungumza kutoa la moyoni ambapo amekiri yeye ni mgumu wa
kukubali lakini hakika Rais Magufuli anafanya mambo makubwa katika nchi
na anastahili kupongezwa.
"Mimi
pamoja na ubishi wangu lakini niseme hadharani nimekukuwa lakini sasa
nimekubali.Niseme amenikosha.Maandiko ya Biblia yanasema huwezi kupendwa
na kila mtu.
"Ukiona
unapendwa na watu wote ujue kuna shida.Pamoja na hayo niseme kazi ambayo
unaifanya kwa ajili ya nchi yetu unastahili sifa na heshima.Wapo
wanaosema ndege zinatokana na kodi zetu wafahamu tunaye Rais ambaye
anatuongoza na kufanya mambo makubwa ndani ya nchi yetu,lazima tukusifu
na kukuheshimu," amesema Askofu Kakobe mbele ya Rais Magufuli.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...