*Asema pamoja na ubishi wake lakini amethibitisha Rais Magufuli anastahili sifa,heshima

  Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

ASKOFU Zacharia Kakobe amesema Rais Dk.John Magufuli anafanya mambo makubwa kiasi cha kwamba amemkosha na kwamba pamoja na ubishi wake kwa sasa anakubali kazi ambayo inafanywa na Rais.

Amesema hayo leo wakati amepata nafasi ya kuomba dua ambapo kabla ya kuomba alianza kwa kuzungumza kutoa la moyoni ambapo amekiri yeye ni mgumu wa kukubali lakini hakika Rais Magufuli anafanya mambo makubwa katika nchi na anastahili kupongezwa.

"Mimi pamoja na ubishi wangu lakini niseme hadharani nimekukuwa lakini sasa nimekubali.Niseme amenikosha.Maandiko ya Biblia yanasema huwezi kupendwa na kila mtu.

"Ukiona unapendwa na watu wote ujue kuna shida.Pamoja na hayo niseme kazi ambayo unaifanya kwa ajili ya nchi yetu unastahili sifa na heshima.Wapo wanaosema ndege zinatokana na kodi zetu wafahamu tunaye Rais ambaye anatuongoza na kufanya mambo makubwa ndani ya nchi yetu,lazima tukusifu na kukuheshimu," amesema Askofu Kakobe mbele ya Rais Magufuli.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...