Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
JEFF Bezos (54) ambaye anashikilia nafasi ya kwanza akiwa mtu mwenye utajiri zaidi duniani akimiliki utajiri wa dola za kimarekani zaidi ya Bilioni 136.2 akimzidi Bill gates kwa dola za kimarekani Bilioni 45 ametangaza kuachana na mkewe MacKenzie Benzos (48) waliyedumu kwa miaka 25 ya ndoa.

Kupitia ukurasa kwake wa Twitter Jeff ameandika kuwa "Baada ya muda mrefu katika mapenzi na kujaribu kuachana  tumeamua kutengana na tutaendelea kuishi kama marafiki" Ameandika Bezos.

Licha ya kutangaza uamuzi huo sababu za kutengana kwao hawajaziweka wazi na inasemekana kuwa talaka hiyo itakuwa ghali zaidi kuwahi kutokea.

Wawili hao walioana mwaka 1993 na kujaliwa watoto wanne huku  MacKenzie akiwa mwandishi huku wakiwa wamiliki wa Amazon.com, kampuni za anga za juu ya Blue Orgin na jarida la biashara la Bloomberg na Washington post.

Jeff alimpiku Gate na kuwa mtu tajiri zaidi duniani mwaka 2017 akiwa na utajiri wa dola za kimarekani bilioni 90.6 na inasemekana Jeff anaweza kuporomoka katika nafasi hiyo kama atatoa nusu ya umiliki wa mali zake kwa MacKenzie.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...