Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kimezindua Kozi ya wahudumu wa ndege ili kuhakikisha uwekezaji wa ndege nchini unaendana na Rasilimali watu wenye ujuzi.

Akizungumza katika uzinduzi wa Kozi hiyo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isaac Kamwelwe amesema kuwa kuna mahitaji makubwa katika Sekta ya anga hivyo vyuo viendelee kuzalisha Rasilimali watu ambao wanaweza kutumika ndani na nje ya nchi.

Mhandisi Kamwelwe amesema upatikanaji wa rasilimali watu katika Sekta ya anga ndani changamoto kutokana na kutokuwepo kwa rasilimali hiyo ilisoma katika vyuo vyetu na kuhitajika kwa watu wa nje ya nchi ambao wanalipwa fedha nyingi.

Amesema kuwa uchumi wa viwanda unategemea na usafiri wa anga katika usafirishaji wa bidhaa katika masoko ya nje kwa haraka zaidi.

Kamwelwe amesema kuwa NIT waendelee kubuni zaidi katika kuzalisha Rasilimali watu wa kuweza kuhudumia ndege zetu na kuacha kutegemea rasilimali inayotoka nje ya nchi.

Nae Mkuu wa Chuo cha NIT Profesa Zakaria Mganilwa amesema kuwa wamejipanga katika uzalishaji wa rasilimali watu katika Sekta ya anga ili kuendana na Uwekezaji wa ndege unaofanywa nchini.Amesema wahudumu ndani ya Ndege ni muhimu sana ambao ndio waangalizi wa usalama wa abiria na mali zao.
 Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isaac Kamwelwe akiwa katika picha ya pamoja na walimu wa kozi ya Uhudumu Ndani ya Ndege.
 Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isaac Kamwelwe akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa kozi ya Uhudumu Ndani ya Ndege.
Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isaac Kamwelwe katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Chuo cha Usafirishaji (NIT)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...