Anaandika Dixon Busagaga,Moshi.

KIKOSI cha  Pikipiki cha jeshi la Polisi mkoa wa Kilimanjaro kimefanikiwa kukamata kilogramu 80 za Dawa za Kulevya  aina ya Mirungi iliyokuwa ikisafirishwa kwa kutumia pikipiki kutoka nchi jirani ya Kenya kuelekea mkoa wa Arusha.

Majani hayo ya Miringi yaliyokuwa yamefungwa katika vifurushi vidogo vidogo zaidi ya 50 na kisha kuwekwa kwenye mfuko mmmoja  mkubwa maarufu kama Kiroba yalipatikana baada ya askari Polisi kujaribu kumkimbiza msafirishaji wa Mirungi ambaye alitekeleza pikipiki na mzigo huo.

Kamanda wa Polisi mkao wa Kilimanjaro ,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamis Issa alithibitisha kukamatwa kwa Dawa hizo za kulevya katika eneo la Uchira ambapo msafirishaji huyo alifanikiwa kukimbia na kuiacha pikipiki aliyokuwa akitumia.

“Mkoa wa Kilimanjaro kumekuwa na tatizo kubwa sana, linalohusiana na usafirishaji wa Mirungi  na wasafirishaji  wamekuwa  wakitumia barabara kuu, sasa askari wa pikipiki  ambao wanafanya kazi hii ya kufukuzana na hawa watu wa mirungi wamefanikiwa kukamata kilogramu 80 za Mirungi”alisema Issah.

Alisema kundi la wasafirishaji wa Dawa hizo za kulevya ambao wamekuwa wakisafirisha kutoka nchi ya Kenya kupitia mpaka wa Holili pindi linapoingia barabarani limeonekana kuwa tishio na hatari kwa usalama wa watu wengine barabarani kwa namna wanavyoendesha pikipiki zao.

“Siku ya leo(Jana) imekamatwa pikipiki moja yenye namba MC 168 CAZ ambayo imetoka nchini Kenya lakini  ni ya Tanzania  na ikiwa na gunia moja kubwa lenye uzito wa kilo 80,nah ii inaonyesha ilikuwa bado  hawajagawana kabisa  lakini askari wetu kwa ushujaa wao wamewafukuza hawa watu  na matokeo yake wamekamata”alisema Issah .

Kamanda Issah alisema  baada ya kufungua mfuko huo walibaini uwepo wa vifurushi vingi vikiwa vimefungwa Majani ya Mirungi kwa njia tofauti tofauti huku ikiwa imepewa majina maalumu ya wahusika wa Dawa hizo.
 MIrungi hiyo naona ilivyohifadhiwa na watuhumiwa hao tayari kwa kusafirishwa. 
 Kamanda wa Polisi mkao wa Kilimanjaro ,Kamishna Msaidizi wa Polisi ,Hamis Issa akionesha Dawa za kulevya aina ya Mirungi walioikamata eneo la Uchira,ambapo msafirishaji huyo alifanikiwa kukimbia na kuiacha pikipiki aliyokuwa akitumia.
 Mirungi iliyokamatwa ikikusanywa na kuwekwa vizuri

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...