Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

SHIRIKISHO la Vyama vya Wachimbaji wa Madini nchini (FEMATA) limefanya ziara ya kutembelea wachimbaji wa Mkoa Dar es salaam na Pwani ambapo wametumia nafasi hiyo kutoa elimu kwa wachimbaji pamoja na kusikiliza kero na kutatua.

Ziara hiyo iliongozwa na Rais wa FEMATA John Bina akiwa ameambatana na uongozi wa chama cha wachimbaji Mkoa wa Dar es salaam na Pwani (DARCOREMA) ambapo pia ujumbe huo ulitembelea wadau wa sekta ya madini wakiwemo wazalishaji na wasambazaji wa vifaa vya wachimbaji vikiwemo Baruti na mitambo ya inayotumiwa na wachimbaji.

Kwa mujibu wa Bina wachimbaji kupitia vyama vyao hawana budi kutatua changamoto zao kupitia meza ya mazungumzo baina hao na Serikali.

Mojawapo ya kero zilizoonekana kukithiri Kwa wachimbaji ni pamoja na wengi wao kukosa mitaji na hivyo kulazimika kuingia ubia na wawekezaji wa Nje makubaliano ambayo Mara nyingi ukosa usawa kibiashara.

Pia Bina amesema tayari shirikisho limeandaa mpango wa namna ya kuwasaidia wachimbaji kutatua changamoto hizo.
 Pichani kati aliyevaa suti nyeusi ni Rais wa FEMATA akiwa wizarani akizungumza na viongozi wa chama cha wachimbaji Mkoa wa  Dar es salaam na Pwani. 
 Baadhi ya viongozi wa Shirikisho la wachimba madini nchini wakipata maelezo baada ya kufanya ziara ya kuwatembelea wachimbaji wa madini Mkoa wa Dar es Salaam
  Baadhi ya viongozi wa Shirikisho la wachimba madini nchini wakiwa kwenye moja ya eno la uchimbaji madini wakipata maelezo kwenye ziara yao kuwatembelea wachimbaji wa madini Mkoa wa Dar es Salaam.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...