*Akiri kumuonea huruma kwani bungeni yupo peke yake,amshangaa kupotosha umma

*Apigilia msumari kwa CAG Profesa Assad,asema asipofika atajua nani muajiri wake

Na Said Mwishehe,Blogu ya jamii

SPIKA wa Bunge Job Ndugai ametoa msimamo wake kwa mara nyingine kuhusu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali(CAG) Profesa Mussa Assad kuwa lazima atafika kwenye Kamati ya Haki,Kinga na Madaraka ya Bunge Maadili huku akieleza kuwa moyo wake unapata taabu sana kwa Mbunge wa ACT Wazalendo Zitto Kabwe.

Akizungumza leo katika Ofisi Ndogo za Bunge jijini Dar es Salaam pamoja na mambo mengine Spika amemzungumzia Zitto kwa kueleza kuwa amekuwa akipotosha umma kuhusu kinga ya CAG."Kuna rafiki yengu mmoja yupo Uganda , kule Uganda CAG ni Ofisa wa Bunge,na Ofisa wa Bunge anaweza kumgomea Spika? Mihimili iko mitatu na niwahakikishie CAG hiyo tarehe 21 atakuja tu.

"Wengi ambao wanaongea kuhusu hili anajua wanatoka upande gani,wapinzani wengi wao wanawaza kupinga tu," amesema Spika Ndugai na kufafanua kama nchi kuna fedha nyingi zinatumika Ubalozi wa Tanzania nchi Marekani kwa ajili ya kuitangaza nchi lakini anatoka Ofisa wa Serikali anakwenda nje kuisema nchi.

"Huwezi kutoka hapa halafu unakwenda kuisema nchi vibaya.Kazi yetu sote ni kuhakikisha nchi inakaa vizuri," amesema Spika Ndugai huku akisema anasikitishwa na namna Zitto anavyopotosha umma."Zitto amekuwa akinipa tabu sana ,niseme tu kutoka moyoni.Pale Bungeni inakuwa rahisi kuwafukuza wabunge wengine wanapofanya makosa maana hata ukiwafukuza wengine wapo lakini Zitto kwenye Chama chao mbunge ni mmoja.

" Hivyo naamua kumuacha tu kwa kutumia busara lakini ukweli huko mbele ya safari nitachoka na niyamchukulia hatua.Bungeni pale watu wanashindana kwa hoja na inaungwa mkono na wabunge wengine."Ndio maana wabunge wakiunga mkono wanne ujue hilo jambo linatupwa na Zitto anakwama kwasababu hana wa kumuunga mkono katika mambo yake,"amefafanua Spika Ndugai.

Ameeleza kwa sasa wabunge wengine wako Dodoma wakiendelea na Kamati za Bunge lakini Zitto yupo Dar es Salaam anahangaika kwenye korido kuhusu kuupinga muswada wa vyama vya siasa." Muswada unaendelea kama kawaida, na ukifika Bungeni utapitishwa .Zitto alitakiwa kuwa kule ili atoe maoni yake ili yafanyiwe kazi,"amesema Spika.

Akifafanua zaidi kuhusu kumuita Mdhibiti na Mkagazi wa Hesabu za Serikali kwenye kamati, amesisitiza lazima aende kuhojiwa na kamati husika na nia njema tu kwani kabla ya kuchukua hatua lazima utoe haki kwa mhusika kupata nafasi ya kujieleza na asipofika atajua nani muajiri wake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...