TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imeiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwenda gerezani kumuhoji mshtakiwa Alloyscious
Mandago katika kesi ya kuisababishia Serikali hasara ya Sh. bilioni mbili inayomkabili yeye na wenzake wanne.
Katika kesi hiyo, mshtakiwa Mandago anashtakiwa pamoja na mfanyabiashara aliyetajwa na Rais John Magufuli kuwa alikuwa akiibia Serikali takriban Sh. Milioni saba kwa dakika, Mohamed Yusufali.
Wakili wa Serikali kutoka Takukuru Leonard Swai Maombi hayo amewasilisha maombi leo, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa.
Wakili Swai alidai, wapo hatua za mwisho za kukamilisha taarifa ili kuwasomea washtakiwa maelezo ya mashahidi(Commital). pia aliiomba mahakama kumuhoji mshtakiwa huyo akiwa gerezani.
Mahakama imeridhia mshtakiwa huyo kuhojiwa na kesi hiyo imeahirishwa hadi Februari 8, mwaka huu itakapikuja kwa ajili ya kutajwa. Mbali na Yusufali na Mandago washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni
Isaack Kasanga, Taherali Sujjauddin Taherali na Mohamed Seif ambapo wanakabiliwa na mashtaka 39 likiwemo la kuisababishia Serikali hasara ya Sh. bilioni mbili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...