Na Anthony Ishengoma-Mara.
Jamii mkoani Mara bado inaendeleza mila potofu ya kuamini kuwa mwanamke asiyekeketwa ni mkosi kwa familia jambo ambalo linaendeleza vitendo vya kwa ukatili wa hali ya juu dhidi ya wanawake Mkoani humo.

Akiongea wakati wa ufanguzi wa Kikao kazi cha uzinduzi wa Kampeini ya kutokomeza ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto   leo Mkoani Mara Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Karolina Mtaphula amesema inapotokea binti anayekeketwa akapoteza maisha kutokana na ukeketaji binti huyo amekuwa akitupwa polini bila kuzikwa kwa taratibu za kawaida kwasababu jamii pia inaamini ni mkosi kwa jamii na kwa familia yake.

Aidha Mtapula aliongeza kuwa Jamii ya Mkoa wa Mara inatakiwa ijilinganishe na mikoa mingine ambayo haina mila ya ukeketaji ili kujenga ufahamu kuwa wanawake kutoka jamii hizo kama wamekuwa wakileta mikosi katika familia zao kama amabavyo mila zao inawafanya waamini.

‘’Wanawake katika Mikoa ambayo haina ukeketaji wanazidi kupiga hatua za kimaendeleo na kufaidika kielimu lakini katika Mkoa wa Mara mila potofu imeendelea kurudisha nyuma maendeleo ya wanawake hivyo nawaomba mlinganishe na jamii hizi kuona kama kweli wanawake wasipokeketwa wanaleta mikosi’’. Alendelea kusema Mtapula.
 Katibu Tawala Mkoa wa Mara Karolina Mtaphula akitoa hutuba yake wakati wa ufunguzi wa kikao kazi kinachoendelea Mkoani Mara kuandaa ujumbe utakaotumika katika mapambano ya kutokomeza ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto.
Afisa Maendeleo ya Jamii  Mkoa wa  Mara  Neema Ibamba akitoa maelezo wakati wa  kuandaa ujumbe utakaotumika katika mapambano ya kutokomeza ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto.
Wajumbe wakikao kazi cha kuandaa ujumbe kwa ajili kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto wakiwa katika picha ya pamoja na Katibu Tawala Mkoa wa Mara Karolina Mtaphula akitoa mara baada ufunguzi wa kikao kazi leo Mkoani humo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...