*Waziri Mkuu apokea maandamano ya wafanyakazi wakimpongeza Rais 
SHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) limeyataka makundi ya wanasiasa kutowatumia wao kama njia ya kujitafutia umaarufu kwa kuzungumzia masuala yao na badala yake wawaachie viongozi wa vyama hivyo kwa sababu wanajitosheleza.

 Pia shirikisho hilo limesema litaendelea kuiunga mkono na kushirikiana na Serikali ya awamu ya tano pamoja na rais wake Dkt. John Magufuli na kwamba watahakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa kuzingatia masharti ya ajira zao.

Hayo yamesemwa leo (Jumatatu, Januari 7, 2019) na Katibu Mkuu wa TUCTA, Yahya Msigwa katika hotuba yake aliyoitoa kwa wafanyakazi baada ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kupokea maandamano ya amani ya vyama vya wafanyakazi.

Watumishi wa taasisi mbalimbali leo wameandamana jijini Dodoma katika viwanja vya Nyerere Squarekwa lengo la kumpongeza Rais Dkt. Magufuli kwa uamuzi wake kufuta kikotoo kipya cha mafao ya wafanyakazi kilichopendekezwa katika kanuni za sheria ya Mifuko ya jamii.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwahutubia watumishi katika maandamano ya amani ya vyama vya wafanyakazi kwenye viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma, Januari 7, 2019.

 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama akizungumza kwenye maandamano ya amani ya vyama vya wafanyakazi katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma, Januari 7, 2019.
 Makamu wa Rais TUCTA Qambos Sule, akizungumza mbele ya watumishi katika maandamano ya amani ya vyama vya wafanyakazi kwenye viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma, Januari 7, 2019.
 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipokea maandamano ya amani ya vyama vya wafanyakazi, yaliyofanyika kwenye viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma, Januari 7, 2019.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwapungia watumishi katika maandamano ya amani ya vyama vya wafanyakazi, yaliyofanyika kwenye viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma, Januari 7, 2019.
 Makatibu Wakuu wakimsikiliza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, wakati akizungumza na watumishi katika maandamano ya amani ya vyama vya wafanyakazi, yaliyofanyika kwenye viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma, Januari 7, 2019. 

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...