Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Joseph Malongo (kushoto) akiendesha kikao kazi cha Makatibu Wakuu kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ). Pamoja na mambo mengine kikao hicho kimejadili juu ya uratibu na ufuatiliaji wa masuala ya Muungano.  Kulia ni Bw. Abdallah Mitawi Kaimu Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais ambae ni Mwenyekiti Mwenza. Kikao hicho kimefanyika hii leo katika Ukumbi wa Hazina, Jijini Dodoma.
 Sehemu ya Wajumbe wa kikao hicho ambao ni Makatibu Wakuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) wakifuatilia kikao hicho. Jumla ya Makatibu Wakuu 26 kutoka Tanzania Bara wamehudhuria kikao hicho.
Sehemu ya Wajumbe wa kikao hicho ambao ni Makatibu Wakuu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) wakifuatilia kikao hicho, kilichofanyika katika Ukumbi wa Hazina Jijini Dodoma. Jumla ya Makatibu Wakuu 13 kutoka Zanzibar wamehudhuria ikiwa ni maandalizi ya kikao cha Kamati ya pamoja kitakachofanyika siku ya kesho Mjini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...