Na Ripota Wetu
KUNDI la Maseneta wa Republican na Democrats nchini Marekani wamesema wamefikia makubaliano ya ufadhili wa Serikali kuelekea tarehe ya mwisho inayotishia kufungwa kwa sehemu fulani ya shughuli za Serikali.

Kwa mujibu wa mtandao wa DW inaeleza kuwa wabunge wanakabiliwa na tarehe ya mwisho Februari 15 ya ufadhili wa Serikali na kuafikiana na mahitaji ya fedha ya rais Donald Trump kuhusu ujenzi wa ukuta na Mexico.

Hata hivyo ikiwa tarehe hiyo ya mwisho itafikiwa bila muafaka, Serikali huenda ikafunga sehemu fulani ya shughuli zake na kuwalazimu mamia kwa maelfu ya wafanyakazi wa shirikisho kufanya kazi bila ya malipo. Vyombo vya habari vya Marekani vimemnukuu seneta wa Republican Richard Shelby kuwa kumefikiwa makubaliano.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...