Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama katikati akitoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali ya Bandari hiyo kwa wafanyabiashara wa Mikoa ya kanda ya Kaskazini waliotembelea na kuvutiwa kupitisha shehena za mizigo yao |
Wafanyabiashara hao wakiendelea kupata ufafanuizi wa masuala mbalimbali
Meneja wa Bandari ya Tanga
Percival Salama kushoto akiwa na Katibu tawala Msaidizi wa mkoa wa Kilimanjaro wakitembelea
eneo la Bandari ya Tanga
Meneja wa Bandari ya Tanga
Percival Salama akizungumza na wafanyabiashara hao
Mwakilishi wa Mkurugenzi mkuu wa Bandari nchini Lydia Mallya
akizungumza ambapo aliwataka wafanyabiashara hao kutumia bandari hiyo
kwani tayari ni bandari ya
viwango vya kimataifa.
Katibu Tawala Msaidizi wa mkoa wa Kilimanjaro akizungumza kulia
ni Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama
Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Kilimanjaro Patrick Shirima akizungumza katika hafla hiyo |
Sehemu ya ujumbe wa wafanyabiashara kutoka mikoa ya Kanda ya
Kaskazini wakifuatilia nyumba anayefuatilia ni Moni Jarufu PRO wa
Bandari ya Tanga akifuatilia mkutano huo
Wadau mbalimbali nao wakifuatilia ziara hiyo
Sehemu ya wafanyabishara wakifuatilia mkutano huo katikati
ni Meneja wa Bohari ya Mafuta ya GBP mkoani Tanga Amour
WAFANYABIASHARA wa Mikoa ya kanda ya Kaskazini wameonesha nia ya
kuanza kutumia Bandari ya Tanga kupitisha shehena ya mizigo yao baada
ya kuridhishwa na mabadiliko makubwa ya mfumo wa utendaji wa Bandari
hiyo.
Wameonesha nia hiyo kwenye mkutano wa siku moja baina ya Uongozi wa
mamlaka hiyo na wafanyabiashara hao na wadau mbalimbali kutoka mikoa
ya Tanga,Kilimanjaro na Arusha.
Katika mkutano huo wafanyabiashara hao waliongozwa na viongozi wa
vyama vya Chemba za Biashara,Kilimo na Viwanda(TCCIA),Katibu tawala
Msaidizi wa oa wa Kilimanjaro na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa
Mamlaka ya Bandari nchini na uongozi wa mamlaka ya Bandari Tanga.
Meneja wa Bandari ya Tanga Percival Salama amefafanua kuwa katika
kuhakikisha bandari hiyo inatoa huduma bora kwa wateja wake imeboresha
miundombinu na mifumo ya utendaji na ulinzi katika bandari hiyo.
Amesema kuwa kutokana na maboresho hayo taratibu za uchukuaji wa
mizigo zinatumia muda mchache tofauti na awali kutokana mamlaka zote
za serikali zinazohusika na Bandari zipo kwenye jengo moja.
" Tunataka kuwaondoa hofu wafanyabiashara kuwa sasa hivi Bandari ya
Tanga ni nzuri,salama kwa mizigo na ni ya uhakika kutokana tumeboresha
kuanzia mifumo ya ulinzi,miundombinu,utendaji kazi na Tehama" alisema.
Alieongeza " Kutokana na maboresho hayo ikiwa mteja atakamilisha
taratibu zote za uchukuaji wa mizigo basi kuanzia mizigo kufika
bandarini atatumia siku tatu tu" alisema.
Katika kusogeza huduma zake kwa wateja wa mikoa ya Kaskazini ya
Kilimanjaro na Arusha tayari uongozi wa mkoa wa Arusha kupitia mkuu wa
mkoa huo Mrisho Gambo ametoa eneo lenye ukubwa wa ekari 500 eneo la
Malula katika wilaya ya Arumeru kwa ajili ya ujenzi wa bandari kavu.
" Wafanyabiashara wa Arusha na Kilimanjaro mtakuwa hamna haja ya kuja
hadi Tanga kuchukua mizigo mtakuwa mnasubiri mizigo yenu huko huko
Arusha sisi tunamiambia gharama zetu tu mnalipia moja kwa moja na sisi
tutajuana na Shirika la Reli( TRC) ambao tunategemea ukarabati wa reli
ukikamilika uwatumie wao" alisema.
Mwakilishi wa Mkurugenzi mkuu wa Bandari nchini Lydia Mallya aliwasihi
wafanyabiashara hao kutumia bandari hiyo kwani tayari ni bandari ya
viwango vya kimataifa.
Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Kilimanjaro Patrick Shirima amesema kuwa
waliikimbia Bandari ya Tanga na kuhamia Bandari ya Mombasa nchini
Kenya kutokana na urasimu uliokuwa unafanywa na taasisi za serikali
zilizokuwa zinahusika na utoaji wa mizigo jambo ambalo lilikuwa
linachelewesha mizigo.
" Leo mmetufumbua masikio kusikia haya mabadiliko sasa tunaahidi
kutumia Bandari yetu kwa ajili ya kuingizia mapato serikali yetu,
kwani neno Bandari ya Tanga tuliisahau kabisa" alisema.
Mwenyekiti wa TCCIA mkoa wa Arusha Walter Maeda aliongeza kuwa kwa
wafanyabiashara wa Arusha wanafahamu kuwa kikwazo kikubwa katika
bandari ya Tanga ni taasisi za serikali katika kuchelewesha mizigo
ndiyo maana waliachana nayo.
" Sisi tuliikimbia Bandari ya Tanga na kuamua kutumia Bandari ya
Mombasa kutokana na nenda rudi zilizokuwa zinafanywa na TRA,TFDA,TBS
kwa kweli walikuwa hawana ushirikiano mzuri hali iliyotuletea tabu
sisi wafanyabiashara " alisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...