Na Estom Sanga-Liwale

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,Mheshimiwa George Mkuchika amesema Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF- ni mojawapo ya vielelezo vya mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tano katika kutekeleza Ilani ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya 2015 inayoelekeza serikali na Wananchi kukabiliana na umaskini.

Waziri Mkuchika ameyasema hayo akiwa katika wilaya ya Liwale Mkoani Lindi ambako pamoja na mambo mengine anakutana na Walengwa wa TASAF ili kujionea namna Walengwa hao wanavyotumia fursa zilizoko kwenye Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini kujiletea maendeleo na kupunguza athari za umaskini miongoni mwao.

“kote nchini ninakofanya ziara kukagua shughuli za TASAF ninashuhudia mabadiliko makubwa katika maisha ya Walengwa jambo ambalo ni zuri na linapaswa kuendelezwa” amesisitiza Mhe. Mkuchika.

Aidha Waziri huyo ametaka Wataalam wa sekta mbalimbali nchini kote kuwa karibu zaidi na Wananchi na hususani Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ili waweze kuboresha zaidi maisha yao na kunufaika na jitihada za serikali.

Akiwa katika kijiji cha Mbonde Katika wilaya ya Liwale Waziri Mkuchicha alitembelea baadhi ya kaya za Walengwa na kujionea namna wanavyotumia ruzuku itolewayo na TASAF katika kuboresha makazi kwa kununua mabati na kuezeka nyumba zao huku wengine wakianzisha shughuli za uzalishaji mali kama ufugaji wa kuku,bata, na kukuza shughuli za kilimo na hivyo kujiongezea kipato.

Kuhusu sekta ya afya,Waziri Mkuchika amekagua jengo la zahanati lililojengwa na TASAF kwa kushirikiana na Wananchi katika kijiji cha Mbonde zahanati ambayo imewaondolea wakazi takribani 400 adha ya kufuata huduma za matibabu mbali ya kijiji chao.Amewaasa Wananchi hao kulitunza jengo hilo ili waendelee kunufaika nalo.

Mapema Waziri Mkuchika akizungumza na Watumishi wa Umma waliopo katika Wilaya ya Liwale,aliwataka watekeleze majukumu yao kwa kuzingatia msingi ya uadilifu na kujituma ili kuondoa kero za wananchi huku akionya kuwa kamwe serikali haitawavumilia Watumishi wanaokiuka misingi ya utawala bora kwa namna yoyote ile. 
Waziri Mkuchika akipata maelezo ya namna jengo la zahanati lililojengwa na TASAF katika kijiji cha Mbonde, Wilayani Liwale mkoani Lindi linavyowanufaisha wananchi wa eneo hilo na vijiji vya jirani.
Waziri Mkuchika (mwenye shati jeupe)akiwa katika nyumba ya mmoja wa Walengwa (kulia kwake)katika kijiji cha Mbonde ,nyumba ambayo imezekwa kwa mabati baada ya kupata ruzuku kutoa TASAF.
Waziri Mkuchika akizungumza na Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na Serikali kupitia TASAF katika kijiji cha Mbonde (picha ya chini).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...