NA MWAMVUA MWINYI, PWANI 

WANANCHI zaidi ya 200 mkoani Pwani,wanadai kutapeliwa fedha milioni 185 ,kwa ajili ya kupatiwa viwanja na kujengewa nyumba kwa gharama nafuu kupitia kampuni ya Vicoba group union Tanzania (VIGUTA). 

Aidha Chamwino huko Dodoma wanadai kuidai kampuni hiyo milioni 61 huku wakikosa kupatiwa nyumba walizolipia kujengewa kwa gharama nafuu.

Aliyekuwa meneja wa Viguta mkoani Pwani,Iddi Kanyalu alikiri kuwepo kwa tetesi hizo na kudai taarifa hizo tayari amezifikisha kwenye vyombo vya sheria ili kufanya uchunguzi na sheria kufuata mkondo wake. 

Alisema,ni kweli walikuwa wananchi wanalipia viwanja kwa bei nafuu na nyumba walikuwa wakilipia kwa asilimia 25 mfano ukitaka kujengewa nyumba ya milioni 25 unalipia milioni 7.5 ambapo wengi walishalipia asilimia 25 na wengine fedha zote kisha kuingizwa mkenge. 

Kanyalu alieleza, utapeli huo umegusa watu ambao wameuziwa viwanja hewa na nyumba ambazo hawajakabidhiwa hadi sasa. 

"Wamenisababishia doa, kwanza mimi ni diwani wa kata ya Kongowe, kutokana na aibu hii na mimi kutohusika, nimeshachukua hatua ya kulifikisha suala hili polisi ili kuchukua hatua zaidi "alifafanua Kanyalu. 

Alipoulizwa kuwa kwanini asigutuke toka alipopewa kazi hiyo hadi kufikia hatua ya kuleta kero na ubabaishaji kwa jamii, Kanyalu alijitetea kuwa kama utapeli ulikuwa wa kimataifa hadi kufikia hatua ya kujitangaza kwa wabunge na kuingia mkataba na baadhi ya taasisi za kifedha hivyo haikuwa rahisi kwake kutambua ubabaishaji huo. 

Baadhi ya wananchi wa Kibaha akiwemo Aidan Mndewa na Kisaken ,walibainisha, kutokana na kudai fedha zao kutokana na kutopatiwa viwanja wala nyumba wanaiomba serikali ifuatilie kampuni hiyo na kuwasaidia kurejeshewa fedha zao. 

Wakati huo huo, msimamizi wa VIGUTA Chamwino huko Dodoma, Hilda Kadunda, ambae pia ni diwani viti maalum alisema wananchi walioingia katika mpango huo Dodoma wanadai milioni 300 na Chamwino wanadaiwa milioni 61 ambapo wapo watu waliouziwa viwanja mara mbili mbili. 

"Ninasimamia Chamwino pia kuna wakati nilikuwa katika mkoa wa Dodoma, mkurugenzi Christina na Mwenyekiti Salmin Dauda wao ndio watia saini lakini tukidaiwa wakipigiwa simu wanazima ama kudai hawapo wanashughulikia masuala mengine "

Kamanda wa polisi mkoani Pwani, ACP Wankyo Nyigesa alipoulizwa juu ya tuhuma hizo kama wahusika akiwemo Mkurugenzi wa VIGUTA Christina Rwebangila na mwenye kampuni hiyo Salmin Dauda kama hatua zozote zimeshachukuliwa kufuatia malalamiko hayo, amedai hajapata taarifa hizo. 

Wankyo alielezea, atafuatilia kwa watendaji wake ili kujua kama wamepata taarifa hizo ili waweze kufanya uchunguzi na kuchukua hatua .
Baadhi ya picha zikionyesha nyumba za sampo zilizokuwa zikidaiwa kujengewa wananchi kwa gharama nafuu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...