Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Watoto, Abdulhakiem Kattan wa Saudia Arabia akizungumza kabla ya shughuli ya utoaji vyeti kwa washiriki wa mafunzo ya kusimamia upumuaji kwa wagonjwa wa ICU.
 Daktari Bingwa wa Watoto wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Evelyne  Assenga akikabidhiwa cheti na Balozi wa Tanzania nchini Saudia Arabia, Hemedi Iddi Mgaza baada ya kumalizika kwa mafunzo ya kusimamia upumuaji kwa wagonjwa wanaolazwa ICU. Wengine katika picha ni wataalam wa afya kutoka Saudia Arabia. 

Akizungumza na washiriki wa mafunzo hayo leo, balozi huyo amesema wataendelea kuandaa mafunzo ya huduma za afya kwa wataalam mbalimbali nchini kwa lengo la kuwajengea uwezo. 

Kauli hiyo imetolewa leo na balozi huyo wakati wa kufunga mafunzo ya siku mbili kuhusu upumuaji kwa wataalam kutoka hospitali mbalimbali nchini ikiwamo Bugando, Hospitali ya Mkoa wa Mbeya, Hospitali ya Benjamini Mkapa na Hospitali ya Mkoa wa Dodoma. 

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Lawrence Museru amesema kwamba Muhimbili itaendelea kutoa ushirikiano kwa wataalam wa afya kutoka Saudia Arabia ili kuhakikisha wataalam wabadilisha uzoefu na wenzao kutoka  Saudia Arabia. 

Mafunzo hayo yameandaliwa na Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kushirikiana na Al balsam Cure and Care International Charity Organization
 Baadhi ya washiriki wakiwa kwenye mafunzo hayo leo.
 Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Watoto, Dkt. Martha Mkony akipokea cheti baada ya kumaliza mafunzo ya kusimamia upumuaji kwa wagonjwa wa ICU kutoka kwa Balozi wa Tanzania nchini Saudia Arabia, Hemedi Iddi Mgaza.
 Daktari Bingwa wa Huduma za Usingizi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya, Dkt. Amos Zakharia akifurahia baada ya kuwa miongoni mwa washiriki waliokabidhiwa cheti.
006: Baadhi ya wataalam walioshiriki mafunzo ya kusimamia upumuaji kwa wagonjwa wanaolazwa ICU.
Sehemu ya washiriki wakiwa kwenye mafunzo hayo leo.
 Mtaalam wa wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU), Peter Bahati akikabidhiwa cheti na Balozi wa Tanzania nchini Saudia Arabia, Hemedi Iddi Mgaza.
 Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Watoto, Dkt. Jenifa Metodi akipongezwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Lawrence Museru baada ya kumaliza mafunzo hayo leo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Prof. Lawrence Museru akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa afya kutoka Saudia Arabia na wenzao kutoka hospitali mbalimbali nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...