Tanga; March 18th, 2019: Benki ya Exim mwishoni mwa wiki iliandaa chakula maalum kwa ajili ya wateja wake jijini Tanga ili kutoa wasaa wa kujadili fursa za kibiashara, mipango ya ukuaji na huduma zitolewazo na benki hiyo katika jiji hilo.
Akizungumza kwenye hafla hiyo iliyohudhuliwa na wadau mbalimbali wa benki hiyo wakiwemo viongozi wa kiserikali, wafanyabiashara wakubwa na wadogo pamoja na wafanyakazi wa benki hiyo, Naibu Ofisa  Mtendaji Mkuu wa  benki ya Exim Bw Jaffari Matundu alisema kupitia hafla hiyo  walilenga pia  kutoa fursa miongoni mwa wateja hao ili waweze kufahamiana na kufungua wigo wa kufanya biashara pamoja.
“Pamoja na kushukuru kwa namna ambayo wateja wetu wamekuwa nasi hadi kufikia mafanikio ya kuikuaji na ubora wa huduma zetu, hafla hii inatoa fursa kwa wateja wetu pia kufahamiana wao kwa wao na hivyo kufungua milango ya fursa baina yao,’’ alisema Matundu.
Alisema ukuaji wa benki hiyo unaoshuhudiwa kwasasa ni matokeo ya ushirikiano baina yake na wateja wake ambao kwa kiasi kikubwa wameonyesha imani kubwa kwa benki hiyo hali ambayo imekuwa ikiiwezesha benki hiyo kubuni huduma bora na rafiki za kibenki ili kulinda na kurejesha imani hiyo kwa wateja wa benki hiyo.
Tangu kuanzishwa kwake mwaka 1997 benki hiyo imezidi kujitanua ndani na nje ya nchi ambapo hivi karibuni ilionesha nia na utayari wa kuinunua  rasmi benki ya UBL Tanzania Limited (UBTL) kwa asilimia 100 baada ya kusainishana barua ya kuonesha nia (Letter of Intent).
“Kwa muda wote wa uwepo wake ndani na nje ya nchi benki ya Exim imekuwa ikijipambanua kwa ubora wa huduma ikilenga kujenga thamani ya uwekezaji kwa wadau wake  na kufikia ukuaji wake kwa kutoa huduma kwa upekee na iliyoboreshwa. Haya yote yamekuwa yakifanikiwa kwa urahisi sababu utekelezaji wake umekuwa ni jumuishi kwa kuwa unahusisha wadau wote kwa majadiliano na wateja wetu kama hivi,’’ alisema.
 Pamoja na mambo mengine hafla hiyo ilipambwa na shuhuda mbalimbali kuhusu ubora wa huduma za benki hiyo kutoka kwa wateja mbalimbali wa benki hiyo.
Meneja Uendeshaji wa Benki ya Exim Bi Doreen Mcharo (katikati)  akizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo  wakati wa tafrija ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki yaExim  kwa ajili ya wateja wake wa jiji la Tanga  iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini humo.

Naibu Ofisa  Mtendaji Mkuu wa  benki ya Exim Bw Jaffari Matundu akizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo (hawapo pichani)  wakati wa tafrija ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na benki yaExim  kwa ajili ya wateja wake wa jiji la Tanga  iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini humo.
Mmoja wa wateja wa benki ya Exim Tanzania jijini Tanga Bi Anna Saimo akizungumza kwenye hafla hiyo.
Mmoja wa wateja wa benki ya Exim Tanzania jijini Tanga Bw Sifaeli Mafunga  akizungumza kwenye hafla hiyo.
Baadhi ya wafanyakazi wa banki  ya Exim tawi la Tanga pamoja na Naibu Ofisa  Mtendaji Mkuu wa  benki ya Exim Bw Jaffari Matundu, kwenye picha ya pamoja mara baada ya hafla hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...