Mkurugenzi
wa Halmashaur ya Manispaa ya Moshi,Michael Mwandezi(katikati) akiwa na
Afisa wa Bonde la Pangani , Segule Segule (Kushoto) kwa pamoja
wakishiriki zoezi la kufanya usafi katika soko la Mbuyuni ikiwa ni
uzinduzi rasmi ya wiki ya Maji .
Baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya manispaa ya Moshi,Bonde la Maji la
Pangani,Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA)
wakishiriki katika zoezi hilo lililofanyika katika masoko ya Manyema na
Mbuyuni.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi,Michae Mwandezi akifagia katika neo la soko la Mbuyuni.
Afisa
wa Maji ,Bonde la Pangani ambao ndio waratibu wa Wiki ya Maji kwa mkoa
wa Kilimanjaro ,Segule Segule akizungumza mara baada ya kukamilisha
zoezi la usafi katika masoko ya Mbuyuni na Manyema.
Baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya manispaa ya Moshi,Bonde la Maji la
Pangani,Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) walioshirki katika zoezi la usafi kwenye masoko hayo.
Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii,Kanda ya Kaskazini.
MKURUGENZI
wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi ,Michael Mwandezi pamoja na Afisa
wa Maji ,Bonde la Pangani Segule Segule wamewaongoza watumishi kutoka
Halmashauri,Bonde la Pangani na Mamlaka ya Maji mjini Moshi (MUWSA)
kufanya usafi katika masoko ya Mbuyuni na Manyema.
Zoezi
hilo lililoanza majira ya saa 12:00 za asubuhi na kudumu kwa saa sita
limefanyika ikiwa ni ishara ya kuanza rasmi Wiki ya Maji Duniani ambayo
hufanyika kila mwaka na kuadhimishwa katika maneo mbalimbali nchini.
Tofauti
na miaka iliyopita ,mwaka huu mkoa wa Kilimanjaro kupitia Ofisi za
Bonde la Maji la Pangani ambao ndi waratibu kwa mwaka huu wameanza
katika eneo la Mazingira ambalo pia ni sehemu ya kazi zinazotekelezwa na
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira na Ofisi za Bonde
kwa kushirikiana na ofisi za Halmashauri.
Akizungumza
mara baada ya kumalizika kwa zoezi la usafi katika masoko ya Mbuyuni na
Manyema ,Ofisa wa Bonde la Maji,Pangani Segule Segule alisema
wamechaguliwa kama taasisi itayoongoza maadhimisho ya wiki ya Maji na
kwa kuanza limefanyika zoezi la usafi na baadae matukio mengine
yatafuata.
kwa
upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya manispaa ya Moshi,Michael
Mwandezi alisema manispaa ya Moshi imekua yenye bahati kutokana na uwepo
wa vyanzo vya maji vinavyotosheleza mahitaji ya mji wa Moshi.
"Mwishoni
mwa mwaka jana manispaa ya Moshi ilipata ushindi sio kwa Tanzania pekee
bali kwa nchi za Afrika MAshariki kuwa ni manispaa inayotoa maji ya
kutosha safi na salama,sisi tunabaraka hiyo lazima tumshukuru
Mungu"alisema Mwandezi.
Alisema
kama ishara ya kuadhimisha wiki ya maji Duniani wameanza kwa kufanya
usafi katika masoko na kwamba hali hii ndiyo imekuwa ikiuweka mji wa
Moshi kwenye ramani ya miji misafi Afrika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...