Mauzo ya moja kwa moja yanazidi kuongezeka Afrika Mashariki wakati vijana wenye ujuzi wa teknolojia wakitafuta fursa mpya za ujasiriamali. 

· QNET, kampuni ya mauzo ya moja kwa moja inaimarisha soko la kanda kwa kutoa bidhaa zenye ubora wa hali ya juu na kukuza ari mpya ya ujasiriamali. 

Mauzo ya moja kwa moja (maafuru kama network marketing) yanakuwa kwa kasi katika eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara ya Afrika na hasa Afrika Mashariki, jambo ambalo kwa kiasi kikubwa limesababishwa na ongezeko la idadi ya watu katika kanda hii pamoja na vijana mahiri ambao kwa mujibu wa taarifa ya Uchambuzi wa Ongezeko la Vijana ya Taasisi ya Maendeleo ya Afrika - sasa Afrika Mashariki ina zaidi ya 45% ya vijana kati ya watu milioni 150 walioko Kenya, Tanzania, Rwanda na Uganda. Wengi wa vijana hawa wana elimu, kwa ujumla wana ufahamu wa teknolojia, wepesi kufuata mienendo mipya, wana hamasa ya kuweka juhudi na fikra za ujasiriamali - jambo ambalo ndio sifa ya awali ya mafanikio endelevu katika biashara ya uuzaji wa moja kwa moja. 

Kwa wanaoanza, mauzo ya moja kwa moja ni wazo la biashara ya kimataifa na linaelezewa kama 'uuzaji wa bidhaa za matumizi au huduma, kutoka kwa mtu mmoja hadi kwa mtu mwingine, mbali na maeneo ya maduka ya kawaida'. Mtindo huu wa mauzo una zaidi ya miaka 100 na mwanzoni kabisa ulianzia huko USA. Leo, sasa karibu takribani watu milioni 117 wanajihusisha nayo. Kwa mujibu wa ripoti ya mwaka 2018 ya Shirikisho la Chama cha Wauzaji wa moja kwa moja Ulimwenguni.(World Federation of Direct Selling Association (WFDSA), mauzo ya moja kwa moja yalizalisha $190 bilioni na karibu nusu ya mauzo yote yametoka katika masoko yanayochipukia: 


Inatosheleza kusema, Afrika ina chukua chini ya 1% ya jumla ya mauzo ya WFDSA lakini wataalamu wanakadiria kwamba soko la Afrika Mashariki linatoa fursa ya kukua kwa wajasiriamali wanaochipukia na hata kwa wale walioajiriwa na wana kiu ya kujipatia kipato cha nyongeza kupitia mauzo ya moja kwa moja. 

Katika kanda ambayo mahitaji ya ajira rasmi yanazidi kuwa na ushindani mkubwa na uhaba wa ajira rasmi, mauzo ya moja kwa moja yanatoa njia mbadala za ajira tofauti na ilivyozoeleka kwa wale wanaohitaji kipato cha ziada au mazingira haya ruhusu ajira. 

Akiongea hivi karibuni wakati akitoa taarifa kwa vyombo vya habari, Biram Fall, Meneja Mkuu wa QNET kwa kanda ya kusini mwa Jangwa la Sahara alisema "QNET imesaidia kuwawezesha maelfu ya watuAfrika, hasa vijana, katika muongo uliopita. Tunaona ongezeko la kukubalika kwa Mauzo ya Moja kwa Moja, na idadi ya watu zaidi ya milioni 200 katika Afrika Mashariki, Mtindo huu ni mtindo unaobadilisha maisha kwa wengi" 

QNET inatoa aina mbalimbali za bidhaa za afya, ustawi na mitindo ya maisha kupitia mifumo yake ya biashara ya mitandao (e-commerce) kwa mamilioni ya wateja katika zaidi ya nchi 100, ikiwa inasaidia watu kuishi maisha bora, na kutoa njia mbadala ya kujipatia kipato kwa yeyote anayehitaji kutumia fursa hii. Kampuni pia ina ofisi na mawakala washirika katika nchi 25 duniani kote, na zaidi ya stoo 50, shughuli za uendeshaji na maduka na wauzaji katika nchi kadhaa duniani. Sasa kwa uwepo wake imara katika Afrika Mashariki, QNET imejidhatiti katika kuendeleza mtindo wa mauzo wa moja kwa moja katika kanda hii. 

Kwa kuongezea QNET pia inarudisha faida yake kwa jamii. Baadhi ya wanufaikaji wa Majukumu ya Kampuni kwa jamii ni pamoja na kituo cha kulelea yatima cha Maunga, na Kituo cha kulele yatima cha Newlife Orphans Home ambavyo vimepokea msaada wa chakula na michango kwa miaka ya hivi karibuni. 

Kwa mujibu wa Biram Fall Meneja Mkuu wa QNET katika Kanda ya Afrika, Kusini mwa Jangwa la Sahara; "QNET ina nia ya kurudisha kwa jamii, Hii ndio sababu kwa nini tumewekeza kwa kiasi kikubwa katika miradi ya uwajibikaji endelevu ya kampuni kwa jamii katika maeneo mbalimbali ya Afrika kupitia katika mkono wetu wa uwajibikaji kwa jamii” alisema Fall. 

QNET Ghana, kwa kupitia RYTHM Foundation, imetoa vifaa maalumu 50 vya kusomea vitabu vya kielektroniki (Kindle e-readers) ambavyo vina vitabu 100 vinavyoendana na tamaduni zao kila kimoja. kwaajili ya wanafunzi wa Nima, eneo lenye watu wa kipato cha chini zaidi ndani ya jiji wa Accra, Ghana. Ilikuwa ni mradi uliofanyika kwa ushirikiano na Worldreader, NGO ya utoaji wa elimu duniani na Achievers Ghana, taasisi ya elimu kwa jamii. 

QNET pia inafanya vizuri katika udhamini wa michezo duniani. Baadhi ya ushirikiano mkubwa wa hivi karibuni unajumuisha kuwa Wauzaji wa Moja kwa Moja wa Klabu ya Mpira wa miguu ya Manchester City na Klabu ya mpira wa miguu kwa wanawake ya Manchester city na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) kwaajili ya ligi ya mabingwa ya Total CAF, Kombe la shirikisho la Total CAF na Total CAF Super Cup kwa mwaka 2018 na 2019. Hapo awali washirika wakubwa walikuwa ni pamoja na Formula One, badminton na zaidi, kutokana na imani thabiti ya kampuni kwamba msukumo, shauku na kufanya kazi katika timu iliyopo katika michezo inaendana na ule wa QNET. 



Manufaa 

Imani thabiti ya QNET kwamba hakuna kinachowezesha zaidi kwa mtu binafsi kama uhuru wa kifedha ambao unatolewa na jitihada katika sekta ya mauzo ya moja kwa moja, na inaamini kwamba watu wa Afrika Mashariki, pamoja na shauku yao na fikra za ujasiriamali, watafurahia kiwango bora cha bidhaa zinazotolewa na QNET na fursa za kibiashara kwaajili ya maendeleo binafsi. 

Mauzo ya Moja kwa Moja yanaweza kuwa ni kazi ya kutosheleza kwa wale ambao wanachagua kuchukua fursa hii kama kazi yao kuu au hata kuchukua kama kazi ya ziada kwa sababu inatoa faida za kifedha kutegemeana na muda na juhudi unazoweka katika kukuza biashara yako. Kwa kuongezea, tofauti na biashara zingine za kawaida ambazo zinahitaji mtaji mkubwa, rasilimali na hata uzoefu, biashara ya mauzo ya moja kwa moja inatoa fursa hii ya biashara yenye gharama nafuu kwa kila mmoja anayehitaji kuianzisha, bila kujali kiwango chao cha elimu au uzoefu. Zaidi ya hayo, mafunzo na maelekezo ambayo wafanyabiashara wanaoanza wanapitia (Wawakilishi wa Kujitegemea au IRs kama ilivyo katika QNET) inawapatia ujuzi wa pekee ambao unapelekea kuwa na ujasiri, kujitambua na hatimae ukuaji binafsi ambao unatambua utaalamu wa mtu kama mjasiriamali aliyekamilika. 

Huenda, manufaa makubwa zaidi ya mauzo ya moja kwa moja katika masoko yanayoibukia kama Afrika Mashariki ni kwamba mtindo huu unakuwa na athari zaidi hapa kuliko katika masoko yaliyoendelea kwa sababu ya athari za kifedha inayoweza kuleta katika maisha ya watu - kutoa fursa za ujasiriamali kwa wote, bila kujali ujuzi au uzoefu, hivyo hatimae kuchangia katika kupunguza umasikini katika jamii. 

Katika mizizi ya QNET kuna falsafa ya RYTHM – Raise Yourself To Help Mankind - ambayo inaongoza jitihada zake zote, na kuendesha kampuni sio tu kubadilisha maisha ya watu duniani kote, lakini pia kushirikiana nao katika kupanua athari hizi. 

Kama alivyosema bwana Trevor Kuna, Mkurugenzi Mtendaji wa QNET "Tunaamini kwamba mafanikio ya kifedha peke yake hayatoshelezi" Ili tuweze kuleta athari, tunahitaji kuendeleza watu kuwa binadamu bora ili waweze kutumia mafanikio yao kuchangia katika jamii zao" 


Changamoto 

Kama ilivyo katika biashara nyingine yoyote Sekta ya Mauzo ya Moja kwa moja pia inakabiliana na changamoto. Changamoto ambayo ni kubwa zaidi miongoni mwa hizi ni kuenea kwa mifumo ya pyramid schemes inayoenda kinyume cha sheria ambayo inaonekana kama makampuni halisi ya biashara ya moja kwa moja, ikiwa inaahidi wawekezaji kuwa watajipatia faida nyingi kupita kiasi iwapo wataunganisha watu wengine. Ukweli ni kwamba hawa 'matapeli' wanatengeneza taswira potofu ya Sekta ya Mauzo ya Moja kwa Moja, jambo ambalo linatengeneza kikwazo kwa makampuni halisi kama QNET kusajili washauri wa kibiashara kuendesha biashara zao halisi na halali. Wakati inapokabiliana na hali kama hizo, QNET inasema inatatua tatizo kwa kuelimisha umma kuwa makini na 'matapeli' kama hao na kuwahimiza kuthibitisha uhalali wa kampuni yeyote kufuatana na kutii kwake kwa kanuni, taratibu na sheria zilizowekwa na bodi zinazosimamia na mamlaka zinazohusika. 

Mpaka kufikia hapa, maelezo kutoka QNET yanasema: "Kampuni yoyote inayokuahidi njia rahisi ya kuwa tajiri inapaswa kuangaliwa kwa tahadhari. QNET kwa mfano, ina maelezo ya kutosha ya mapato yanayopatikana kwenye tovuti yake na vifaa vya mauzo. Kampuni za Masoko ya mtandao zinatoa bidhaa zenye ubora au huduma tofauti na mifumo ya pyramid schemes ambayo haina bidhaa halali au huduma. Kampuni bora ya Masoko ya mtandao huwa inatenga kiwango kikubwa cha rasilimali kwaajili ya utafiti na uendelezaji, kutengeneza bidhaa zenye ubora ambazo zina matumizi halisi kwa watu wakati mifumo ya pyramids scheme huwa haifanyi hivyo" 

Inaongeza: "Kampuni za masoko ya mtandano yana sera na taratibu sahihi, pamoja na kanuni za maadili za masoko. Kamuni yoyote halisi ya masoko ya mtandao ina lengo la kufikia ukuaji endelevu kwa kukuza utamanuni wa masoko ya kimaadili. QNET inaweka msisitizo mkubwa katika kanuni za maadili za utendaji kwa wawakilishi wake wa kujitegemea (IRs) na kuwapatia miongozo ya kina kuhusu masoko ya kitaalamu pamoja na sera na taratibu". 

Kusisitiza uhalali wa mauzo ya moja kwa moja, utafiti wa hivi karibuni uliofanywa na Taasisi ya Ngazi Mbalimbali za Masoko ya India (India Multi-Level Marketing Institute) ilichunguza uendeshaji wa aina mbalimbali kama vile Avon, Mary Kay, QNET na Tupperware na kubaini kwamba 'sio mifumo ya scheme) ya aina ya piramidi au aina nyingine yoyote. 

Changamoto nyingine inayoikabili sekta ya mauzo ya moja kwa moja ni ujuzi ambao haujaendelezwa hasa kwa wale ambao wamechukua fursa hii hivi karibuni. QNET inasema kwamba inatatua changamoto kwa kuweka msisitizo mkubwa sana katika mafunzo na elimu kwa IRs. Mafunzo hayo sio tu kamba yanaendeleza ujuzi wao wa kitaalamu lakini pia unalenga katika ukuaji na maendeleo binafsi. 

Ni wazi kwamba, kufikisha bidhaa katika maeneo ya vijijini na maeneo ya mbali ni kikwazo kingine lakini QNET imeweza kutatua hili kwa kuajiri IRs ambao wanatengeneza mtandao ndani ya jamii zao kwaajili ya kurahisisha upatikanaji na pia kuwasaidia kuagiza mzigo mkubwa kwa punguzo kwa lengo la kutoa mzigo, hivyo kuhakikisha usambazaji endelevu wa bidhaa. 

Kuingia kwa QNET katika soko la kanda inaweza pia kukabikiana na ushindani kutoka kwa kampuni ambazo tayari zilishaanzishwa za bidhaa za reja reja na nembo za kimataifa lakini mtindo wake wa pekee wa usambazaji utaiweka QNET tofauti na kutengeneza njia ya mafanikio. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...